BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

JESHI LA POLISI LAPIA MAFURUKU VIKUNDI VYA KANGAMOKO NA KIGODORO, KISA NI.......

http://freemedia.co.tz/daima/wp-content/uploads/2014/06/kangamoko.jpgMKUU wa Jeshi la Polisi nchini, (IGP) Ernest Mangu, amepiga marufuku vikundi vya ngoma vya Kigodoro, Kangamoko na vingine vinavyokiuka maadili ya kitanzania.


Kutokana na hatua hiyo, IGP Mangu amewaagiza Makamanda wa Polisi wa mikoa yote nchini  kuhakikisha wanadhibiti vikundi hivyo vinavyodaiwa kuwa chanzo cha matukio mbali mbali ya kihalifu na kuporomosha maadili.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini SSP Advera Senso, kwa niaba ya  IGP Mangu, alisema vikundi hivyo vinatakiwa kufuata taratibu zinazowekwa na halmashauri zao pasipo kukiuka maadili.

Alisema licha ya vikundi hivyo kufanya vitendo vya kukiuka maadili ya kitanzania pia wakati wa ngoma hizo wahusika wamekuwa wakifunga barabara na kufanya uhalifu katika maeneo wanayofanyia burudani zao hali inayosababisha usumbufu mkubwa kwa watu wengine.

“Hatupingi ngoma za asili bali tunakataa vitendo vinavyodhalilisha utu wa binadamu hasa mwanamke na maadili ya kitanzania, vinalindwa. Hili sisi kama jeshi hatuwezi kulivumilia,”alisema Senso.

Alisema hata matukio mengi ya kihalifu yanayohusisha makundi ya kihalifu kama Panya Road, Mbwa mwitu na Machizi sabini ni matokeo ya ngoma hizo zinazokesha kwa kucheza nusu uchi.

Juni 18 mwaka huu wacheza ngoma wawili wa kundi la Kangamoko wakazi wa Mwananyamala, walijeruhiwa kwa risasi na watu wanaodhaniwa kuwa ni askari baada ya kutokea vurugu za kuwazuia askari wasitekeleze wajibu wao wa kuzuia ngoma hizo kama zilivyotangazwa na mamlaka husika.

Mbali na kupiga marufuku ngoma za vigodoro,  Senso alisema Polisi imeanzisha operesheni maalum ya kuwadhibiti madereva piki piki, bajaji, guta na baiskeli wanaokiuka sheria za barabarani na kusababisha ajali za mara kwa mara na kuathiri nguvu kazi ya taifa.

Alisema miongoni mwa makosa yanayofanywa na madereva wa vyombo hivyo ni pamoja na kutozingatia alama na michoro ya usalama barabarani, kupita taa nyekundu inayoawaashiria kusimama pamoja na kuendesha piki piki zao kwa mwendo wa hatari, jambo aliloeleza kuwa ni kinyume na sheria za usalama barabarani.

Katika siku za hivi karibuni baadhi ya vikundi vya ngoma vinavyojitambulisha kwa majina kama Vigodoro, Kanga moko (Ndembendembe laki si pesa), Kantangaze na Bunyero bunyero inayochezwa kwenye baadhi ya kumbi maarufu za burudani, vimekuwa vinara wa kukiuka maadili ya kitanzania kwa kucheza wakiwa uchi.

Kutokana na uchezaji huo wa kukiuka maadili mijadala mbali mbali ya namna vikundi hivyo vinavyochangia kuporomosha hadhi ya mtanzania hasa wanawake, zimekuwa zikijadiliwa hata kufikia hatua ya bunge kuhoji hali hiyo.

Wakati wa kujadili bajeti ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa mwaka wa fedha 2014/15, baadhi wabunge waliihoji serikali kwanini imekaa kimya wakati utamaduni wa kitanzania umekuwa ukipotoshwa hadharani pamoja na kuchochewa kwa hisia za ngono na makundi hayo.TANZANIA DAIMA
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: