BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

OPERESHENI YA UTUMBO WA MTOTO PACHA YAFANIKIWA.

 
Daktari wa watoto mapacha waliokuwa wameungana akiwa amewabeba mara baada ya kufanywa upasuaji hivi karibuni.

Dar es Salaam. 
Hatimaye mtoto Eliud, mmoja kati ya pacha waliokuwa wameungana kabla ya kutenganishwa kwa upasuaji huko India Februari, mwaka huu, ameanza kwenda haja kubwa kwa njia ya kawaida baada ya kufanyiwa upasuaji mdogo na kurudishwa ndani sehemu ya utumbo iliyokuwa imetoka nje.
Upasuaji huo ulifanywa Ijumaa iliyopita katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na jopo la madaktari bingwa kutoka Misri.Baada ya kurejea kutoka India na kisha kwenda Mbeya, Eliud alipata tatizo la utumbo mkubwa kutoka nje na kutopenda kula, hali iliyomfanya adhoofu.
Jana, baba mzazi wa pacha hao, Eric Mwakyusa alisema upasuaji huo ulifanikiwa na sasa mtoto huyo anaendelea vizuri... “Ninamshukuru Mungu sasa Eliudi anakula na kwenda haja kubwa kwa njia ya kawaida. Kwa sasa tunauguza kidonda tu.”
Daktari anayewasimamia watoto hao, Zaituni Bokhary hakupatikana kuzungumzia hali za pacha hao lakini Mwakyusa alisema madaktari hao wako karibu na pacha hao kujua maendeleo yao.
Mwakyusa alisema pacha mwingine, Elikana ambaye pia alikuwa na tatizo la utumbo kutoka nje kwa kiasi kidogo ikilinganishwa na Eliud, atafanyiwa upasuaji... “Kurudisha utumbo ndani na kuziba tundu.”
Watoto hao wanatarajiwa kurejea India Agosti, mwaka huu kwa ajili ya upasuaji mwingine.MWANANCHI
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: