BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

RAIS UHURU KENYATTA ARUDI KWA KISHINDO KATIKA MAHAKAMA YA KIMATAIFA YA UHALIFU ICC.

 
Rais Kenyatta akipokelewa na naibu wake William Ruto

Mamia ya watu kwa shangwe na vigelegele wamemkaribisha Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta baada ya kurejea kutoka kikao chake katika mahakama ya kimataifa ya ICC mjini the Hague.


Kenyatta alihudhuria kikao maalum katika mahakama hiyo Jumatano, na kuwa Rais wa kwanza aliye mamlakani kufika katika mahakama hiyo.

Mahakama hiyo ilimtaka afike mbele yake kutokana na malalalmsihi kutoak kwa kiongozi w amashitkaka kuwa serikali ya Kenya inaficha ushahihidi kuhusiana na kesi inayomkabili.

Kenyatta alikwenda Hague kwa kikao maalum na mahakama ya ICC.


Alikanusha madai ya uhalifu dhidi ya binadamu wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi nchini Kenya mwaka 2007 ambayo yalisababisha vifo vya watu 1,200 na kuwaacha wengine zaidi ya laki sita bila makao.

Kenyatta alipokelewa na idadi kubwa ya watu waliokuwa wanacheza densi pamoja na gwaridde la heshima.

Asubuhi na mapema, wafuasi wake walipanga foleni kwenye barabara ya kutoka uwanja wa kimataifa wa ndege mjini Nairobi.

 

Rais Kenyatta katika mahakama ya kimataifa ya ICC
Walipeperusha bendera na kusikika wakiimbia kwa shangwe na kumsifgu Kenyatta wakisema kuwa Rais wao hana hatia.

Rais aliwahutubia kwa mda mfupi umati huo wa watu ambao waliombwa kufika kumpokea rais na waziri wa usalama.

Mwandishi wa BBC aliyefika kushuhudia Rais huyo akiwasili nchini alisema kuwa Kenyatta ana wafasui wengi.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: