BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

SUA YATWAA KOMBE LA SOKA UMISETA NGAZI YA MANISPAA YA MOROGORO 2015.



Mshambuliaji wa timu ya soka ya kanda ya SUA, Fidoline Chendi akitafuta mbinu za kuwatoka walinzi wa timu ya kanda ya kati, Ally Katanga na Shakuru Maulid wakati wa mchezo wa fainali mashindano ya UMISETA ngazi ya kanda ya Manispaa ya Morogoro, Kanda ya SUA iliibuka na ushindi wa penalti 10-9 baada ya sare ya bao 1-1. 


Juma Mtanda, Morogoro.

Mashindano ya kusaka wachezaji wenye vipaji ya umoja wa michezo kwa shule za sekondari Tanzania (UMISETA) ngazi ya kanda ya Manispaa ya Morogoro yamemalizika kwa timu ya soka ya wavulana ya kanda ya SUA ikitawazwa mabingwa kwa mwaka 2015 mkoani hapa.



Timu ya soka kanda ya SUA chini ya kocha wao mkuu, Emmanuel Kimbawala maarufu kama Mourinho alilazimika kutumia kila aina ya mbinu ndani ya uwanja kwa mifumo tofauti tofauti katika mchezo wa fainali dhidi ya Kanda ya Mjini Kati ili kuweza vijana wake kuibuka kidedea kwa kupata ushindi wa changamoto ya mikwaju ya penalti ya bao 11-10.



Katika mchezo huo wa fainali timu ya soka ya Mjini Kati ndiyo iliyoanza kupata bao katika dakika ya 20 lililofungwa na mshambuliaji, Christopher Adam huku SUA wakilazimika kusawazisha katika dakika ya 90 kupitia kwa, Michael Jeromeh na kufanya mchezo huo kumalizika kwa sare ya bao 1-1.



Mwamuzi chipukizi wa mchezo huo, Raphael Ikambi aliamuru kupigwa penalti kama kanuni za mashindano hayo ili kupata mshindi ambapo timu ya Mjini Kati ilipata penalti tisa wakati wenzao SUA wakipata penalti 10, baada ya Joseph John kufunga penalti yao ya mwisho kufuatia, Abdul Shomari kukosa penalti ya 10.



Kwa upande wa soka la wasichana, kanda ya Tungi iliibuka mabingwa kwa changamoto ya penalti baada ya kushinda penalti 2-1 dhidi ya Bigwa kufuatia kumaliza dakika 90 kwa sare ya 0-0.





Katika mchezo wa netiboli, kanda ya Mjini Kati ilitwaa ubingwa huo baada ya kufikisha pointi 10 na vikapu 130 ikifungwa vikapu 60 wakati katika mchezo wa wavu wavulana kanda ya Tungi pia ilitwaa ubingwa huo wakati Kihonda A ikitwaa taji kwa upande wa wasichana.



Kwa mchezo wa basketiboli, kanda ya Mjini Kati ilishinda taji  baada ya kuilaza Kihonda B kwa vikapu 44-39 katika mchezo wa fainali huku kwa mpira wa mikono wavulana Kihonda B ilishinda taji hilo kwa kufikisha pointi tisa na wasichahana kanda ya Mjini Kati ikitawazwa mabingwa.


Baada ya kumalizika kwa michezo hiyo ya kanda, zaidi ya wachezaji 64 wa michezo mbalimbali wamechaguliwa kabla ya kuchujwa kuunda timu zitakazo shiriki michezo ya UMISETA ngazi ya mkoa wa Morogoro ambao watawakilisha mkoa huo katika ngazi ya taifa.

Michezo ya UMISETA ngazi ya mkoa wa Morooro inatarajiwa kutimua vumbi Mei 27 mwaka huu katika uwanja wa jamhuri mkoani hapa.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: