BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

NDEGE YA KIVITA YA TANZANIA (JWTZ) YATUMBUKIA BAHARI YA HINDI NA MARUBANI WAWILI WAKATI WAKIFANYA MAZOEZI DAR ES SALAAM.


Moja ya ndege za kivita zinazotumiwa na majeshi. Picha ya Mtandao.


MARUBANI wawili wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), wanahofiwa kufa maji baada ya ndege yao ya mazoezi, kuangukia katika mwambao wa Bahari ya Hindi eneo la Visiwa vya Mbudya, Kaskazini Mashariki mwa Jiji la Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa ya Kurugenzi ya Habari na Mahusiano ya JWTZ Makao Makuu, ajali hiyo ilitokea jana majira ya saa 3.30 asubuhi. 


Ilisema mara baada ya ajali hiyo, marubani wake, Luteni Kanali Talkisiyo Bruno Ndongoro na Kapteni Gaudence Peter Hamis walipotea.

Taarifa hiyo iliongeza kuwa, chanzo cha ajali hiyo ni hitilafu ya injini, jambo ambalo limeelezwa marubani hao walipoligundua, walifanya juhudi za kujiokoa kutoka katika ndege hiyo, kwa bahati mbaya waliangukia baharini na kuzama. 


Kutokana na tukio hilo, JWTZ imetoa taarifa ikisema inaendelea kuwatafuta marubani hao kwa kutumia boti za kijeshi.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: