BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

NI GIZA NENE AJALI YA KUANGUKA KWA HELIKOPTA YA CCM MBUGA YA SELOUS MOROGORO, MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA LUDEWA DEO FILIKUNJOMBE NA RUBANI JE WAMEFARIKI DUNIA ?.

chopa 2Headlines za kisiasa kwa Tanzania zimetawaliwa na ajali ya Helikopta ya CCM ambayo imeanguka katika hifadhi ya wanyama ya Selous ambapo Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu alithibitisha kwamba mmoja wa abiria aliyekuwemo ndani ya helikopta hiyo ni Mgombea ubunge jimbo la Ludewa, Deo Filikunjombe (CCM).
Leo mapema mgombea wa ubunge kupitia CCM jimbo la Ukonga, Jerry Silaa alipost picha ya Helikopta na kuandika maneno kuhusiana na ajali hiyo.

"Baba yangu Capt.William Silaa akiwa na Mhe, Deo Filikunjombe na abiria wengine walipata matatizo ya engine ya helicopter 5Y-DKK jana jioni wakitokea Dar kuelekea Ludewa. Taarifa za mwisho ilionekana imeanguka kwenye msitu wa Selous. Hakuna mawasiliano ya simu. 


Kutokana na tukio hilo vyombo vya ulinzi na usalama vya serikali usiku kucha wa jana kuamkia leo viliendelea na jitihada za kufika eneo la tukio na jitihada kubwa zaidi ziliendelea.
 

Ajali hiyo imetokea katika kitalu cha wawindaji kinachojulikana kama R3 ambapo walioshuhudia wakiwa katika kitalu R2 tofauti yao ni kwamba wametenganishwa na mto ambao maji yake yanaenda kwa kasi huku kukiwa mamba"alisema Waziri Nyalandu.

“Sisi tulichokifanya kama Serikali ni kwamba tumetuma kikosi kimoja ambacho kilikuwa kina askari nane huku Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Leonard Paulo naye akituma askari kwenda kwenye eneo hilo la ajali.


Taarifa ya awali ya tukio hilo baada ya waziri kupata taarifa ilieleza kuwa....“Taarifa tulizozipata kutoka kwa mashuhuda wa eneo hilo kwa wawindaji mahiri walipiga simu kwa njia ya Satelite na kueleza kuwa wameona helikopta moja imeaguka katika msitu wa Selous kwenye kitalu R3 jirani na mto Ruaha baada ya hapo kisha wakaona moto ukiwaka.”alisema Nyalandu katika taarifa yake fupi.Chanzo Millardayo.com
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: