BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

ROSE MHANDO AOMBA KUJIUNGA NA CCM DODOMA

Baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu, mwanamziki wa nyimbo za injili nchini Rose Mhando ametumbuiza katika mkutano wa Halmashauri Kuu CCM unaoendelea mjini Dodoma, kisha kuomba kujiunga na chama hicho tawala.

Awali Katibu wa Uenezi na Itikadi wa CCM, Humphrey Polepole akimkaribisha jukwaani kutumbuiza, aliwatangazia wajumbe wa mkutano kuwa Rose Mhando na kundi lake atapanda jukwaani kutumbuiza na baada ya hapo, atawasilisha ombi lake la kutaka kujiunga na chama hicho tawala.

Rose aliimba wimbo wa kusifu utendaji wa Rais John Magufuli na kibwagizo kinachomalizikia na maneno ...”tuna imani nawe.” Rose Mhando, alipomaliza shoo’ yake,wajumbe wa mkutano huo kutoka mikoa yote hapa nchini waliinua mabango yao na kumshangilia.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: