![](https://ichef.bbci.co.uk/news/660/cpsprodpb/3858/production/_99342441_b359ee50-e16e-49c9-91b2-b999a20c66ca.jpg)
Mashua moja iliyokuwa imebeba takriban watu 140 waliyokuwa safarini kwa shughuli ya kidini iligongana na boti iliyokuwa na watu 65.
Usafiri wa nyakati za usiku umepigwa marufuku katika ziwa Tanganyika.
Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Sweetbert Njewike, wanaendelea kuwatafuta watu ambao hawajaonekana waliokuwa wakisafiri na vyombo hivyo.
Alisema shughuli za uokoaji zinafanywa kwa pamoja na vikosi vya Polisi, Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na wananchi.
Kulingana na gazeti la mwananchi mkuu wa Wilaya ya Uvinza, Mwanamvua Mrindoko amesema kuwa uchunguzi wa awali unaonyesha kwamba kulikuwa na dosari zilizosababisha ajali hiyo.
Alizitaja dosari hizo kuwa ukosefu wa vifaa vya uokoaji, vya kuzima moto mbali na boti kufanya safari za usiku.
0 comments:
Post a Comment