BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

HABARI MPYA !!!!!!!! MBUNGE WA ROMBO APATA AJALI, MAMA YAKE ADAIWA KUPOTEZA MAISHA PAPO HAPO.

TAARIFA YA KUSIKITISHA.

 
Mbunge wa Rombo-Kilimanjaro Mhe, Joseph Roman Selasini amepata ajali ya ya gari huku mama yake mzazi akiripotiwa kupoteza maisha iliyotokea katika eneo la Boma Ng'ombe mkoani Kilimanjaro.

Taarifa kutoka kwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro, Absalom Mwakyoma zinasema kuwa Mhe Selasini alikuwa akiendesha gari yake huku ikidaiwa kuwa na watu sita ambapo kati yao watu watatu hali zao zikielezwa kuwa ni mbaya.


Kamanda huyo akiongea na waandishi wa habari kwa simu ya alisema kuwa kwa sasa hawezi kuthibitisha kwamba ni watu wangapi wamepoteza maisha katika ajali hiyo na kuongeza kuwa majeruhi wote wamekimbizwa katika hospitali kwa ajili ya kupatiwa huduma.

Mwakyoma alisema kuwa taarifa zaidi atazitoa muda mfupi  baada ya kujua hali halisi ya tukio hilo kwani kwa sasa yuko njiani akielekea eneo la tukio kisha kwenda hospitali kuangalia majeruhi wa ajali hiyo.

Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: