BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

WAKE WA OSAMA BIN LADEN WATUMIKIA KIFUNGO CHA SIKU 45.

Mmoja wa wake wa Osama Bin Laden.
Wakili wa wajane wa Osama Bin Laden na mabinti zake Atif Ali Khan ameeleza kuwa familia hiyo imepewa kifungo cha siku 45 kila mmoja kwa kuishi nchini Pakistan pasipo bila kibali. 

Khan aliyasema hayo wakati akizungumza na shirika la habari la BBC na kueleza kuwa wanawake hao wameanza kutumikia vifungo vyao na wanatarajiwa kurejeshwa nyumbani kwao katika majuma mawili yajayo.

Wajane wawili ni raia wa Saudi Arabia huku mwenzao wa tatu akiwa mzaliwa wa yemen. 
Wakili huyo alisema kuwa wameshauriana na serikali ya Saudi Arabia kuwakubalia wajane wawili kurejea nyumbani huku mjane anayetoka Yemen akikubaliwa kurudi nyumbani.

Wajane watatu walichukuliwa na maafisa wa usalama baada ya Osama Bin Laden kuuawa katika operesheni ya kikosi maalum cha Marekani nchini Pakistan hapo mwezi Mei.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: