BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

UKITIMIZA VIGEZO HIVI UNAPATA MCHUMBA MWENYE BIKRA RAIA WA CHINA MIAKA 38.

MWANAMKE mmoja nchini Uchina ambaye ni mwanaharakati wa kutetea wasichana kubaki bikra hadi waolewe, ametoa tangazo kwenye mtandao akitafuta mume.

Mtandao wa rednet.cn umeripoti kuwa mwanamama huyo mwenye umri wa miaka thelathini na nane aliandika tangazo hilo kwenye wavuti uitwao Sina Weibo.

Mwanadada huyo anayejulikana kwa jina la Tu, aliandika vigezo anavyovitaka ambavyo mume huyo awe navyo.

Amesema lazima awe mwanachama wa chama kinachotawala nchini China, au awe mfanyakazi wa serikali. Aidha amesema iwapo mchumba atapatikana, hakutakuwa na tendo la ndoa kabla ya ndoa, na vile vile hakuta kuwa na tendo hilo pia hadi miaka mitatu ya baada ya harusi.

Ujumbe huo wa Dada Tu, umezua sokomoko na kusomwa na zaidi ya watu elfu kumi katika kipindi cha saa moja tu. Baadhi ya wachangiaji wa sakata hilo wamesema kwa vigezo hivyo kamwe hatopata mchumba.

Kwa mujibu wa Mwanamama Tu ambaye anatokea jimbo la Hubei, amesema hana muda tena wa kusubiri mchumba kwa njia za kawaida na ndio maana ametoa tangazo hilo kwenye mtandao.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: