BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MBUNGE WA JIMBO LA MOROGORO MJINI MHE, ABOOD AKABIDHI PIKIPIKI TANO ZENYE THAMANI YA SH800,000 WAKATI WA UZINDUZI WA CHAMA CHA WAENDESHA PIKIPIKI MANISPAA YA MOROGORO.

 
 Mbunge wa jimbo la Morogoro mjini Abdullaziz Abood akijari kuwasha moja ya pikipiki tano alizotoa kwa chama cha waendesha pikipiki Manispaa ya Morogoro zenye thamani ya sh800,000 wakati wa uzinduzi wa ofisi na katiba ya chama hicho katika mtaa wa Simu kata ya Mjipya mkoani hapa, kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa chama hicho, Anamwikira Massawe na mwenye kofia ni katibu Juma Bega.
 Mhe Abood akimkabidhi mwenyekiti wa chama cha waendesha pikipiki Manispaa ya Morogoro ], Anamwikira Massawe kadi ya pikipiki katika sherehe hizo, na kushoto ni katbu wa chama hicho Juma Bega.
 Mhe akikata utepe ikiwa ishara ya ufunguzi wa ofisi hiyo.
Akizungumza na wanachama wa chama cha waendesha pikipiki muda mfupi baada ya uzinduzi huo.
Sehemu ya wageni waalikwa akiwemo mwandishi wa gazeti la Mwananchi Lilian Lucas kulia akichukua dondoo kwa ajili ya habari.
 Wanachama wa chama hicho wakifuatilia matukio yaliyokuwa yakiendelea katika uzinduzi huo.
Moja ya pikipiki ikiwa imebebwa juu mara baada ya kutelemshwa kutoka kwenye gari (halipo pichani) kabla ya kuanza shughuli za uzinduzi wa chama hicho na katiba.

Na Lilian Lucas,Morogo
WAENDESHA pikipiki maarufu kama bodaboda katika manispaa ya Morogoro wametakiwa kutokuwa chanzo cha vifo vya watu na badala yake kuwa waadilifu na wenye kutii sheria za usalama barabarani.

Mbunge wa jimbo la Morogoro mjini Abdullah Azizi Abood alitoa kauli hiyo jana wakati wa uzinduzi wa ofisi na katiba ya chama cha wawendesha bodaboda pikipiki manispaa ya Morogoro CHAWAPIMAMO ambapo alisema kumekuwa na tabia ya baadhi ya waendesha bodaboda hao kusababisha vifo kwa abiria wao kwa kupata ajari na hata wakati mwingine kuwaua kwa kudhania kuwa wana mali.

Abood alisema ni vyema waendesha bodaboda hao wakawa na tabia ya kuaminika kwa watu wanaowabeba,uadilifu na kujiweka katika hali ya usafi ikiwa  ni pamoja kuwaeshimu askari wa usarama barabarani.

Pia mbunge huyo aliwataka viongozi wa CHAWAPIMAMO kuongoza kwa kufuata katiba na wawe wenye kutoa taarifa za mapato na matumizi mara kwa mata katika vikao vyao ili kuwepuka minung’uniko isiyokuwa ya lazima kutoka kwa wanachama.

“Kuanzishwa kwa chama hiki kusiwe chanzo cha migogoro hasa ninyio viongozi msiwe wenye kuabudiwa na mnajiona kama miungu watu kwa wenzetu kwani hiki ni chama cha wananchama fanyeni kazi kwa kufuata misingi mliojiwekea,”alisema

Akisoma risala katika uzinduzi wa chama hicho katibu wa CHAWAPIMAMO Juma Bega alisema kuwa chama kilianzishwa 2009 kikiwa hakina ofisi na kwamba mpaka sasa kina wanachama zaidi ya 400 ambao ni waendesha bodaboda,kimekuwa kikishirikiana na jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani kutoa mafunzo juu ya usalama na udereva kwa waendesha bodaboda hao.

Bega alisema kuwa kuanzishwa kwa chama hicho kumesaidia kukuza ajira na kipato kwa vijana,biashara kuongezeka pamoja na kupunguza ajari za mara kwa mara za barabarani.

Alisema mamlaka ya mapato Tanzania TRA pamoja na kuondoka kodi mapato katika pikipiki kumekuwa na changamoto inayokabiliana ambayo ni kutozwa ghalama kubwa ya kodi ya leseni ya barabara (Motor vehicle Licence) na kilalamikia kutakiwa kuweka mtungi wa gesi ambao hawaoni sehemu ya kuuweka.

Aidha alisema matarajio yao ni kuanzisha mfuko wa kusaidiana nia ikiwa ni kusaida pale mwenzao anapopata ajari ama kufariki kutokana na chombo anachokiendesha pikipiki ama vinginevyo.

Katika uzinduzi wa ofisi na katiba cha chama hicho mbunge Abood alitoa msaada wa pikipiki 5 aina ya TOYO yenye thamani ya shilingi 8 milioni ambazo alizitoa kambo chanzo cha mapato cha chama hicho ambapo aliwataka kukopeshana na kuzalisha.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: