BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

RAIS KABILA AMTIMUA KAZI MKUU WA JESHI LA NCHI KAVU DRC.

 
Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo amemsimamisha  kazi kwa muda Mkuu wa Jeshi la Nchi Kavula nchi hiyo, baada ya Umoja wa Mataifa kumtuhumu Jenerali Gabriel Amisi Kumba kuwasaidia waasi na makundi yanayobeba silaha dhidi ya serikali ya Kinshasa. 

Hata hivyo serikali ya Kongo imeanzisha uchunguzi wa kina kubaini tuhuma hizo zilizotolewa na Umoja wa Mataifa dhidi ya Jenerali Gabriel Amisi Kumba za kuwasaidia waasi wa nchi hiyo.
 
Kwa upande mwengine, wakati waasi wa mashariki mwa Kongo wakizidi kusonga mbele katika eneo hilo, Jean Marie Runiga Lugerero kiongozi wa waasi wa March23 ameelekea Kampala mji mkuu wa Uganda kwa shabaha ya kufanya mazungumzo na Rais Yoweri Kaguta Museveni wa nchi hiyo juu ya mgogoro wa mashariki mwa Kongo. 

Waasi wa M23 jumanne iliyopita waliudhibiti kikamilifu mji wa Goma, makao ya Jimbo la Kivu na Kaskazini na hivi sasa wanasonga mbele kuelekea upande wa kusini mwa mji huo.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: