BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

SERENGETI BOYS YAILAZA CONGO BRAZZAVILLE KWA KUITANDIKA 1-0

 
Wachezaji wa Serengeti Boys, Hussein Twaha (shoto), Joseph Lubasha na Selemani Hamis Bofu wakibadilioshana mawazo wakati wakitoka mapumziko

TIMU ya taifa ya vijana ya Tanzania 'Serengeti Boys' imejiweka njia panda baada ya kuichapa Congo Brazaville bao 1-0 katika mchezo wa kwanza wa kusaka tiketi ya kufuzu kushiriki Fainali za Mataifa ya Afrika kwa vijana mwakani.

Chipukizi Mudathiri Yahya aliifungia Serengeti Boys bao pekee katika dakika ya 15 kwa mpira wa adhabu uliompita kipa wa Congo Brazaville, Ombandea Mpea katikati ya miguu 'tobo' na kujaa wavuni.

Kwa matokeo hayo sasa Serengeti Boys watalazimika kufanya kazi ya ziada kulinda ushindi wao huo watakapokuwa jijini Brazaville wiki mbili zijazo kwenye mchezo wa marudiano ili kukata tiketi ya kwenda Morocco.

Selemani Hamis Bofu  akitafuta mbinu za kumtoka beki wa Congo Brazzaville, Tmouele Ngampio

Kocha Jacob Michelsen alisema mchezo ulikuwa mgumu kwa vijana wake, lakini anawashukuru kwa kupata ushindi huo.

"Nimefurahi tumeshinda ingawa ni ushindi mwembamba, sasa tunahitaji kujiandaa vizuri zaidi kwa ajili ya mechi ya marudiano," alisema Michelsen.

Serengeti Boys sasa inahitaji ushindi au sare yoyote ili iweze kurudia rekodi yake ya mwaka 2003 walipokata tiketi ya kwenda Gambia, lakini waliondolewa kushiriki kwenye michuano hiyo na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) baada ya kubainika walitumia wachezaji waliozidi umri akiwamo Nurdin Bakari wa Yanga.

Katika mchezo wa jana, Congo walionekana kucheza kwa kujiamini na kutumia pasi fupifupi, lakini ngome ya Serengeti ilikuwa makini kujilinda na kufanya mashambulizi ya kushtukiza.

Katika dakika  ya 14 mchezaji Seleman Bofu wa Serengeti Boys aliangushwa nje kidogo ya eneo la 18 na beki wa Congo hivyo  mwamuzi Miiro Nsubuga kutoka Uganda alitoa adhabu iliyopigwa na Mudathiri na kwenda moja kwa moja wavuni na kuamsha shangwe kwa mashabiki wachache waliojitokeza uwanjani hapo.

Baada ya bao hilo, Congo waliamka na katika dakika ya 26 bado kidogo wangepata bao la kusawazisha baada ya mpira wa kona wa Ibara Vinny kuunganishwa kwa kichwa na Obassi Gambo na kupaa juu kidogo ya lango la Serengeti.

Katika dakika ya 32, mchezaji Hussein Ibrahim wa Serengeti Boys aliwatoka mabeki wa Congo na kupiga shuti lililodakwa na kipa Mpea.

Vijana wa Congo walitawala sehemu kubwa ya mchezo huo, lakini washambuliaji wake walikosa mbinu za kuipenya ngome ya Serengeti Boys ambao wenyewe walikuwa wakicheza kwa kujihami na kutumia mipira mirefu na kushambulia kwa kushtukiza.

Kipindi cha pili vijana wa kocha Michelsen walirudi uwanjani kwa kasi zaidi na katika dakika ya 59 shuti la Mudathiri la umbali wa mita 35 lilitoka sentimita chache.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: