BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

WAZIRI WA ULINZI NCHINI URUSI AFUTWA KAZI

Aliyekuwa waziri wa ulinzi wa Urusi Anatoly Serdyukov
Aliyekuwa waziri wa ulinzi wa Urusi Anatoly Serdyukov kataka midotcomnewsindonesia.wordpress.com.

Rais wa Urusi Vladimir Putin amemfuta kazi waziri wa ulinzi kwa kashfa ya rushwa, badiliko ambalo ni la kustusha tangu serikali ya chama cha Kremlin kurejea madarakani kwa muhula wa tatu huku chama hicho kikizidi kupoteza imani.

Putin ameziba pengo la waziri Anatoly Serdyukov ambaye amekuwa akitekeleza mageuzi ya kijeshi yasiyo maarufu ingawa yaliungwa mkono na chama cha Kemlin kwa kumpa nafasi hiyo gavana wa zamani wa jimbo la Moscow na waziri wa mambo ya dharura Sergei Shoigu.

Wachambuzi wanasema kwamba kufutwa kazi kwa afisa huyo wa juu ambaye amenufaika na uungwaji mkono usio na masharti wa rais Putin ni hatua inayolenga kuwatia hofu wasomi wakati rais huyo anapo pambana na mgogoro mbaya wa kisiasa katika miaka takriban 13 ya uongozi wake.

Putin aamesema kuwa Serdyukov, mmoja wa watu watatu nchini Urusi wenye uwezo wa kupata namba ya kianzio ya uzinduzi wa nyuklia, ameondolewa katika wadhifa wake ili kupisha uchunguzi dhidi ya tuhuma za rushwa ya dola. 


Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: