Kwa ufupi
Kila mtu ana haki ya kwenda mahakamani, tupo tayari kupokea ushauri lakini hatupo tayari kupokea vitisho.http://www.mwananchi.co.tz
Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.
Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.
DAR ES SALAAM.
MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba amesema ofisi yake inafanya na itaendelea kufanya kazi kwa kuzingatia Sheria ya Mabadiliko ya Katiba iliyopitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na si vinginevyo.
MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba amesema ofisi yake inafanya na itaendelea kufanya kazi kwa kuzingatia Sheria ya Mabadiliko ya Katiba iliyopitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na si vinginevyo.
Kiongozi huyo ametoa kauli hiyo siku moja baada ya
tishio la asasi ya Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata) kwenda mahakamani
ili kusimamisha mchakato wa Katiba Mpya.
Akizungumza ofisini kwake jana, Jaji Warioba
alisema kama kuna watu wanataka kwenda mahakamani kupinga mchakato huo
wanaruhusiwa kufanya hivyo.
Alisema mbali ya kufuata sheria, Tume yake
inafanya kazi kwa kuzingatia maoni yaliyotolewa na wananchi zaidi ya
300,000 pamoja na makundi maalumu 16
0.
0.
“Kila mtu ana haki ya kwenda mahakamani, tupo
tayari kupokea ushauri lakini hatupo tayari kupokea vitisho,” alisema
Jaji Warioba, ambaye pia amewahi kuwa Waziri wa Sheria na Mwanasheria
Mkuu wa Serikali.
Alisema maelezo yalitotolewa jana na Jukata hayana
msingi wowote na kusema jukwaa hilo linakwenda mahakamani kujishtaki
lenyewe na si Tume ya Mabadiliko ya Katiba kwa kuwa inafanya kazi zake
kwa mujibu wa sheria.
“Nina shaka sana na matamko yanayotolewa na jukwaa
hili, zipo asasi ndani ya jukwaa hilo ambazo zimeiomba Tume kushiriki
katika Mabaraza ya Katiba bila kivuli cha Jukata. Sasa Jukwaa hili ni
nani haswa?” alihoji.
Alisema kauli kuwa tume hiyo inaminya mchakato wa
Katiba si ya kweli akisema imeundwa kwa kuzingatia mapendekezo ya
makundi mbalimbali na inafanya kazi yake kwa kufuata sheria na
inawajumuisha watu wenye weledi na uadilifu mkubwa.
“Wanaosema kuwa sisi tunaipendelea CCM maana yake
ni kwamba wanabeza uteuzi wa tume hii ambayo uwepo wake umeridhiwa na
wananchi wote kupitia katika makundi yao.
Waliotakiwa kuiponda kwamba inafanya kazi bila kuzingatia weledi ni wananchi ambao walikutana na wajumbe wakati wakitoa maoni yako katika mikoa mbalimbali nchini,” alisema.
Waliotakiwa kuiponda kwamba inafanya kazi bila kuzingatia weledi ni wananchi ambao walikutana na wajumbe wakati wakitoa maoni yako katika mikoa mbalimbali nchini,” alisema.
Alisema kwa mujibu wa sheria, Tume hiyo imepewa
miezi 18 kukamilisha kazi yake na Oktoba mwaka huu ndipo itakamilisha
rasimu ya Katiba, kabla ya kuanza kwa Bunge Maalumu la Katiba na baadaye
kupigiwa kura ya maoni.
“Tunatakiwa tulaumiwe baada ya kuitoa rasimu ya
Katiba, lakini kwa sasa ni kama tunaingiliwa kazi yetu kwa sababu hakuna
mtu anayejua rasimu itakuwaje na hakuna anayejua Tume itapendekeza nini
kiwemo kulingana na maoni ya wananchi, hasa suala la Muungano na
madaraka ya Rais,” alisema.
Alisema Tume yake itaendelea na ratiba yake kama
kawaida na kwamba mchakato mzima wa Katiba utasimamishwa iwapo tu
Mahakama itasikiliza hoja za Jukata na kuziona zina msingi.

0 comments:
Post a Comment