BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

ZITTO KABWE ADAIWA KUTAKA KUKWAMISHA BAJATI YA WIZARA YA NISHATI NA MADINI KWA MWAKA WA FEDHA 2013/2014..



http://www.wavuti.com/uploads/3/0/7/6/3076464/547749302.JPG?689MBUNGE wa Kigoma Kaskazini Zitto (Chadema) Kabwe ameonyesha nia ya kupinga ama kuikwamisha hotuba ya bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kutokana na hatua ya Serikali kugawa vitalu vipya kabla ya kuwepo kwa sera na sheria mpya ya madini.

Taarifa za ndani kutoka kwa watu wa karibu na Mbunge huyo zinadai kwamba mbunge huyo anajiandaa kuandaa utaratibu wa kupinga bajeti hiyo mpaka serikali itakapo leta sheria mpya, “Serikali imegawa nakala za bajeti ya Nishati na Madini na wabunge wote wanatakiwa kuhu
dhuria semina hiyo, lakini chakushangaza ni kwamba nakala zote zimeandikwa kwa lugha ya Kiingereza"kilisema chanzo hicho.

Mbali na mtoa taarifa hiyo kudokeza Habarimpya.com juu ya suala hilo Mbunge huyo pia aliandika taarifa za kikao hicho katika ukurasa wake wa Facebook na kudai kwamba hatua hiyo ya serikali inapaswa kupingwa kwa nguvu zote.

"Kati ya Wabunge waliopinga hatua hiyo ni pamoja na Zitto Kabwe ambaye alisema kwamba Gesi Asilia ipo kwenye rasimu na tayari imetangaza tena kugawa vitalu vya  mafuta na gesi  kaskazini mwa Ziwa Tanganyika.endelea kupitia na kukopi  audifacejackson blog."Haraka hii ya serikali kugawa vitalu bila sera wala Sheria inatoka wapi? 

Nitashangaa sana wabunge kukimbilia posho za semina hii na kuhalalisha maamuzi yasiyo zingatia maslahi ya Taifa kwa vizazi vya sasa na vijavyo"alisema Zitto na kuongeza:

 "Uamuzi wa kugawa vitalu vipya bila kwanza kuwepo kwa sera na sheria mpya unapaswa kupingwa kwa nguvu zote.kwani inabidi tuangalie ni wapi tunakwenda na kwa manufaa gani baadae sio tu tuwe tunakimbilia posho".
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: