BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

BAADA YA KIFO CHA MWANAYE MWANAMUZI LANGA KILEO, MAMA MZAZI AONGEA JUU YA KIFO CHICHO. SIKIA HAYA MANENO



 
MAMA wa marehemu Langa Kileo, Vanessa Kimei (pichani) amefungua kinywa chake na kusema kifo ni mipango ya Mungu lakini kama angekuwepo nyumbani kwake Mikocheni, Dar, mwanaye asingekufa haraka kiasi hicho.

Akizungumza na Amani hivi karibuni, Mama Langa alisema wakati mwanaye alipoanza kuugua hadi kupatwa na umauti Juni 13, mwaka huu, yeye alikuwa safarini nchini Marekani kum
uona mwanaye mwingine aliyekuwa amejifungua.

“Wakati mwanangu ameanza kuumwa sikuwepo, nilikuwa safarini Marekani nilikoenda kumuona mwanangu wa kike aliyekuwa amejifungua, kwa mila za kwetu ni lazima mama kwenda kumuogesha mtoto lakini ningekuwepo mwanangu asingeondoka jamani,’’ alisema mama Langa.

Akifafanua kauli yake, mama huyo alibainisha kuwa kipindi alipokuwa akiishi na mwanaye kabla hajasafiri, mara nyingi alikuwa akimhudumia alipokuwa akiumwa hivyo hata katika ugonjwa uliosababisha mauti yake basi angeweza kumtibu yeye mwenyewe.

Alisema kuwa wakati mwingine alikuwa akimuwekea hadi dripu za dawa akiwa pale nyumbani na kunusuru maisha ya mwanaye lakini ghafla kifo kimetokea wakati yeye hayupo.

“Nilikuwa namuwekea dripu za dawa mwanangu hapahapa nyumbani, alikuwa anaugua kwa muda na kisha anarudi katika hali ya kawaida,” alisema kwa uchungu mama Langa.

Hata hivyo baadhi ya waombolezaji waliokuwepo msibani walimsihi mama huyo kukubaliana na mipango ya Mungu kwamba kila mwanadamu lazima atakufa, hali iliyompa faraja na kumfanya anyamaze.
Marehemu Langa aliyefariki baada ya kusumbuliwa na kile kilichoelezwa kuwa ni ugonjwa wa malaria kali na homa ya uti wa mgongo, alizikwa Jumatatu iliyopita katika Makaburi ya Kinondoni, Dar. 
Na Mwaija Salum wa GPL.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: