KAMA OFISI ZA WANAUSALAMA ZINAKAGULIWA KWA NAMNA HIYO WATU WENGINE HALI IMEKUWAJE !.OFISA mmoja wa Usalama wa Marekani (FBI), hivi karibu wakati wa ziara ya Rais Barack Obama akiwa na mbwa aliingia Makao Makuu ya Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam na kufanya ukaguzi.
Tukio hilo lilitokea muda mfupi kabla ya msafara
wa magari ya Marekani kupita yakitokea Ikulu kwenda Uwanja wa Ndege wa
Julius Nyerere kumlaki Rais Barack Obama.
Polisi ambaye hakutaka kutajwa alisema ofisa huyo aliingia na mbwa hadi maeneo ya mapokezi, lakini muda mfupi walitoka.
“Walikwenda moja kwa moja map
okezi wakafanya ukaguzi, kisha wakatoka nje ya jengo na kama hiyo haitoshi, ofisa huyo akiwa na mbwa alikwenda sehemu ya kuegesha magari yenye kesi na yale ya kawaida na kuanza kufanya ukaguzi, baada ya hapo waliondoka,” alisema polisi huyo na kuongeza.
okezi wakafanya ukaguzi, kisha wakatoka nje ya jengo na kama hiyo haitoshi, ofisa huyo akiwa na mbwa alikwenda sehemu ya kuegesha magari yenye kesi na yale ya kawaida na kuanza kufanya ukaguzi, baada ya hapo waliondoka,” alisema polisi huyo na kuongeza.
“Licha ya mimi kutokuwa na cheo pale, lakini hili
la kutukagua na mbwa, ni kama wametudhalilisha... sisi ndiyo
tunaaminika kwa usalama, leo hii wanatukagua na mbwa. Tena Kituo Kikuu.”
Hata hivyo, usalama kwenye vituo vingi ikiwamo
Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Juliusu Nyerere, vilikuwa chini ya
usimamizi na uangalizi wa makachero wa Marekani.
CHANZO MWANANCHI.
CHANZO MWANANCHI.

0 comments:
Post a Comment