BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MJUE MZEE ABDULLAH ALRUWEIHY ALIYETEMBEA KWA MKUU KUTOKA DAR HADI TANGA. NO 3.

Alipofika kule Tabora akawakuta waarabu wenziwe akina Hamed bin Said ruweihy.Akawauliza jee vipi  hapa?.Wakamwambia eeh bwana tafadhali sana kwa hisani yako hakuna njia wala la kufanya kimbilia kwenye meli  ya wabelgiji.Nenda zako mpaka Ujiji.Ukifika ingia kwenye meli yao.
 
Akatoka Tabora mpaka Ujiji.Kufika Ujiji  ipo meli.Akaingia mpaka Kongo.Kufika Kongo moja kwa moja akaenda akaukumbatia mlingoti wa bendera ya Ubelgiji.Akaulizwa haya nini shida yako?.Akasema shida yangu mimi bwana nafukuzwa na Muiengereza,na sijui akanipata kama ataniwacha hai au ataninyonga.
   Akaambiwa hapa hapana Muiengereza wala mdachi wala nani atakayeweza kukupata. Kaa kitako.Baada ya kukaa kidogo ndipo alipopiga simu kwa jamaa zake Tabora.
Swali:Ni mji gani wa Kongo alipokaa?.
Jibu:Ni mji wa Kasongo,Kongo.Alipiga simu kwa Nassor bin Muhammed akawaambia kwa haraka sana nileteeni mwanangu kwa sababu hali yangu ni dhariri sasa.Kwa maana alipofika goti lilikuwa limevimba halifanzi kazi kutokana na mwendo na dhiki iliyompata.Kweli nikachukuliwa nikapelekwa Kongo nikamuwahi marehemu baba.
Swali:Katika Familia yenu mlikuwa muko wangapi?
Jibu:Kwa hapa Afrika alikuwa kanizaa mimi peke yangu.
Swali:Turudi Kongo.
Jibu:Nilipofika Kongo tukaonana na marehemu baba lakini kwenda hawezi tena.Akasema jee umefika mwanangu,akachukua kalamu na karatasi akaandika .
Kulikuwa na bwana mmoja wa Kisangani akiitwa Salim bin Amraan Al Maamry na mwengine akiitwa Nassor bin  Salim  AlHarmy ,alikuwa mtu mkubwa katika Kongo.
Akawaambia  nawakab
idhi mwanangu huyu.Pindi nikiwa hai ninaye mwenyewe,lakini  pindi Mwenyezi Mungu akinipa mauti basi asiwekwe pahala popote .Fanzeni hima apelekwe mpaka Unguja halafu apelekwe Oman.
Kweli  haikuchukua muda mkubwa Mwenyezi  Mungu akamukhitarisha,na mimi sikuwa na maisha ya kuketi pale tena.
Watu wakafanza utaratibu wakanipakia ndani ya meli mpaka Kigoma.Kufika Kigoma nikapakiwa ndani ya garimoshi  mpaka Darisalama.
Kufika Darisalama  nikaja mpaka Unguja  nikakaa mwaka mmoja kwa baba yetu mdogo,sheikh Suleiman bin Said Alruweihy.
Swali:Ni eneo au mtaa gani huko Unguja?
Jibu : Ni Michungwa miwili.Baada ya muda huo baba yangu mdogo akatoka Muscat kuja kunichukua.Jina lake ni Abdulla bin Habiib bin Salim Alraawahy.
Tukaenda mpaka Oman nikakaa miaka niliyokaa.Wengine wanasema nilikaa miaka 14 au 15.
Swali:Ulipotoka kule Oman kurudi Unguja mlitumia usafiri gani?.
Jibu:Usafiri tuliotumia ni jahazi.Sembuku moja ya watu wa Samail  baatin huko Udama.Huyo nahodha jina lake Yussufu.
Nakumbuka siku hizo hakuna riali,ilikuwa inatumika kursh.Nililipa kursh saba,nikapewa kikaratasi tu.Hakuna siku hizo kupiga picha na nini na nini !,hakuna wakati ule.
Siku zile mtawala wa Oman alikuwa sayyid Said bin Taimuur.Akasema sayyid Said hapa pana gunia saba za zabibu zinahitaji kupakiwa  zipelekwe Dhofar  halafu nyie mwende zenu.Tukapakia.
Dhofar ndiyo hii sasa inayoitwa Salala na mfalme Qaboos.
Tulipofika tukateremsha nikaulizwa wee mtoto mdogo wenda wapi?.Nikasema Yaa sayyid anaa adh-habu ilaa daar Zinjibaar.Nikajibishana nao kwa kiarabu kujitetea kuwa baba yangu amefariki na mama yangu yuko Zinjibaar.
Mwishowe nikaruhusiwa.Nikaambiwa;Marhaban bika.Hayya idh-hab yash-haduka Rahmaan.
Tukatoka moja kwa moja mpaka tukafika Zanzibar.Kufika sikukaa sana nikaenda mpaka Tabora kumtizama mama yangu.Nikamkuta bado mama yu hai.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: