BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

RAIS BARACK OBAMA ASABABISHA ABIRIA WENGI KUACHWA KATIKA MABASI YA MIKOANI.

http://t3.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcR7eKgp0n40MxPYYSdylOI_dYoP3d8sMDV0FMepecsbKvAFAIbnRAIS BARACK OBAMA.
DAR ES SALAAM. 
MABADILIKO ya ratiba za mabasi yaendayo mikoani na nje ya nchi yanayoanzia safari zake Kituo Kikuu cha Mabasi, Ubungo (UBT), yamesababisha abiria wengi kushindwa kusafiri huku wengine wakiagizwa kwenda Kimara mwisho.
Mwananchi iliyofika Kituo cha Mabasi Ubungo saa 11:30 asubuhi,  ilielezwa na mmoja wa wafanyakazi wa mabasi ya Air Force, Ipyana Mwamlenga, kuwa waliagizwa na Sumatra kuhakikisha mabasi yote yawe yameondoka kituoni hapo  ifikapo saa 1:00 asubuhi.
“Tuko katika mchakamchaka, tunatakiwa kuondoka hapa hadi saa 1:00 asubuhi ...unajua tulishaamua kuwa hakuna usafiri leo kutokana na barabara kufungwa, lakini tukaamua tuondoke nyuma ya muda wa kawaida,” alisema.
Gazeti hili lilishuhudia idadi kubwa ya mabasi yakitoka kituoni hapo kuanzia saa 12:30 asubuhi, huku ask
ari wa usalama barabarani wakihimiza madereva kuondoka haraka ili wasilete usumbufu  barabara itakapofungwa.
Baadhi ya abiria walionekana kupigwa butwaa baada ya kukuta mabasi waliyotakiwa kusafiri nayo kuondoka.
“Wasubuiri hawa wanakuja huko, wote wana tiketi,” alisikika mwanamke mmoja akiwasiliana na wahusika wa mabasi ya Prinses Muro, lililoondoka mapema.
Habari zilizopatikana jana asubuhi kituoni hapo, abiria waliokuwa wasafiri kwa mabasi  yanayoanzia safari zake zaidi ya saa 1:00 asubuhi, walitakiwa kwenda Mbezi.
Hata hivyo, mabasi yaliendelea  kutoka kituoni hadi saa 1:40 asubuhi.
Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpiga, alisema mabasi na malori yote yanayotoka mikoani yatazuiwa Kibaha hadi saa 7:00 mchana.
Mpiga aliwataka wasafiri wanaoelekea mikoani kuhakikisha wanawahi kwa sababu ratiba za mabasi zilikuwa zimebadilika.
CHANZO MWANANCHI.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: