BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

HII NDIYO SABABU YA MWENYEKITI WA CHADEMA TAIFA NA MNADHIMU WA KAMBI YA UPINZANI BUNGENI KUKAMATWA WAKATI WAKIELEKEA BUNGENI MJINI DODOMA LEO MKOANI IRINGA LEO.


VIONGOZI waandamizi wa chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) Taifa akiwemo mwenyekiti wao Bw Freema Mbowe, Mbunge wa Singida Mashariki ambae ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni Tundu Lissu na mwenyeji wao mbunge wa jimbo la Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa wakamatwa na polisi mkoani Iringa Viongozi hao wamekam
atwa   leo majira ya saa 3 asubuhi kati kati ya mji wa Iringa wakati wakitokea eneo la Kihesa kuelekea Bungeni mjini Dodoma kwa shughuli za kibunge kabla ya jeshi la polisi kuwatia matatani na kuwafikisha kituo cha polisi.
 Akithibitisha kukamatwa viongozi hao kamanda wa polisi wa mkoa wa Iringa Ramadhan Mungi alisema kuwa viongozi hao walikamatwa kwa mahojiano kutokana na kutoa kauli hatarishi kwa amani wakati wa mkutano wao uliofanyika katika uwanja wa Mwembetogwa kwa ajili ya mabaraza ya ukusanyaji wa maoni ni rasmu ya katiba.
 Kamanda Mungi alisema kuwa kibali ambacho Chadema walipewa kilikuwa kikianza saa 9 Alasili hadi saa 12 .;00 ila wao waliendelea na mkutano huo hadi majira ya saa 12 .25 na kila walipofuatwa zaidi ya mara moja kuelezwa kuhusu muda wa kibali chao kuisha bado viongozi hao waliendelea kuendesha mkutano huo huku wakitumia vipasa sauti kutoa maneno ya dhahaka dhidi ya jeshi la polisi. 

Hata hivyo alisema kuwa jeshi la polisi lilishindwa kutumia nguvu kwa kuwakamata ama kuwashusha viongozi hao jukwaani wakati wa mkutano huo kama njia ya kuepusha vurugu ambazo zingeweza kutokea iwapo nguvu zingetumika kuwashusha kwa kuvunja sheria za nchi .Chanzo Matukio Daima.

 "Tunawashikilia viongozi hao kutokana na kutoa kauli hatarishi wakati wa mkutano wao wa jana (juzi) uliofanyika uwanja wa Mwembetogwa ....kwani kibali chao kilikuwa kikiisha saa 12 .00 jioni ila wao walizidisha muda na maofisi wa polisi waliokuwepo waliwafuata na kuwakumbusha juu ya muda waliopewa katika kibali chao ila wao badala ya kusitisha mkutano walitumia kipasa zauti kujibu na kutoa kauli cha hatarishi ....Jeshi la polisi lilitumia busara na kuwaacha hadi walipomaliza na asubuhi tuliwakamata kitaalam bila ya kutokea vurugu zozote"

Alisema kuwa viongozi hao hadi majira ya saa 5  leo  asubuhi walikuwa wakiendelea kuhojiwa na jeshi la polisi na kuwa kufikishwa ama kutofikishwa mahakamani kutajulikana mara baada ya mahojiano hayo .
Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Iringa Suzana Mgonakulima alisema kuwa jumla ya waliokamatwa jana ni viongozi wanne akiwemo Mbowe, mbunge Msigwa , Lissu pamoja na diwani wa kata ya Mvinjeni katika Manispaa ya Iringa Frank Nyalusi .

Mngonakulima alilitaka jeshi la polisi kutimiza wajibu wake bila kutumiwa na chama chochote cha siasa ama mtu yeyote katika shughuli zao kwani kwa kufanya hivyo ni kuondoa imani ya polisi na wananchi.

Kuhusiana na kumamatwa na kuachiwa kwa viongozi hoa alisema kuwa viongozi hao waliachiwa majira ya saa 5.30 asubuhi baada ya kuhojiwa kwa zaidi ya masaa matatu ambapo kila mmoja alitakiwa kuthaminiwa na mtu mmoja kwa dhamana ya Tsh milioni 2 na wote walikidhi masharti ya dhamana na kuruhusiwa kuendelea na safari hadi hapo watakapotakiwa kufika polisi .
" Tunawashangaa sana polisi Iringa Chadema kuzidisha muda dakika 5 imekuwa tatizo mbona CCM wamekuwa wakifanya mikutano yao hadi saa 1 usiku bila viongozi wake kukamatwa ....Chadema hatuna tatizo kwa kuonewa na huu si mkutano wa kampeni ni mkutano wa kukusanya maoni ya katiba ambao hatutapewa muda kamili na tume ...ila tunawasamehe bure polisi"alisema mwenekiti huyo wa Chadema Iringa mjini.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: