BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

HIVI NDIVYO WANARIADHA WALIVYOCHUANA KUWANIA MEDALI KATIKA MASHINDANO YA TAIFA YA RIADHA MOROGORO.





MOROGORO. 
WANARIADHA Rose Seif na Tumain Elisha jana waliuongoza Mkoa wa Pwani kutwaa medali za dhahabu kwenye fainali ya kuruka chini mruko mmoja (long jump) na kuruka chini miruko mitatu (tripple jump) kwenye mashindano ya riadha ya taifa yaliyomalizika jana kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini hapa.
Tumain ndiye alikuwa wa kwanza kutwaa dhahabu kwenye fainali ya long jump akiruka umbali wa mita 4 na cm 64.Ushindi wa Pwani uliendekezwa na Rose Seif kwen
ye fainali ya tripple jump akiruka umbali wa mita 10 na cm 16.
Medali ya pili kwenye tripple jump ilichukuliwa na Tumain aliyeruka mita 10 na cm 00 na Rose akichukua medali kama hiyo kwenye long jump akiruka mita 4 na cm 54.
Nafasi ya tatu kwenye tripple Jump ilichukuliwa na Suzan Msoka wa Mwanza aliyeruka umbali wa mita 9 na cm 93.
Kwenye tripple jump upande wa wavulana, Michael Gwandu wa Manyara aliibuka kinara akiruka umbali wa mita 13 na cm 09, huku Micheal Danford wa Kilimanjaro akikamata nafasi ya pili akiruka mita 13 na cm 29 na Denis David wa Kagera akichukua medali ya tatu ya Shaba akiruka umbali wa mita 13:19.
Kwenye fainali ya mita 10,000 ya wavulana, Ezekiel Jafari wa Kagera akiibuka kinara akitumia dakika 30:07:37, huku Joseph Theophil wa Arusha akikamata nafasi ya pili (30:08:70) na Paulo Itambu wa Singida akikamata nafasi ya tatu (30:13:90).
Mita 5000, Alphonce Felix wa Kagera alikuwa wa kwanza kwa kutumia dakika 14:35:15, huku Joseph Theophil wa Arusha akitwaa medali ya Fedha (14:34:50) na Nyangero Patrick wa Kagera akikamata nafasi ya tatu (14:43:59).
Mita 400, Rose Seif wa Pwani aliibuka kinara (1:03:20), huku Filomena Magine wa Mwanza akikamata nafasi ya pili (1:04:87) na nafasi ya tatu, Yedida Paulo wa Shinyanga (1:06:42).
Mita 100, Laurent Masatu wa Arusha aliibuka kinara akitumia sekunde 10:82, Taratibu Machaku wa Tanga nafasi ya pili sekunde 11:01 na Adinan Haruna wa Kilimanjaro sekunde 11:03.
Katika fainali ya mita 400, Rose Seif wa Pwani aliibuka kinara akitumia dakika 1:03:20, Filomena Magine wa Mwanza akitwaa medali ya fedha dakika 1:04:87 na Yedida Paulo wa Shinyanga akikamata nafasi ya tatu dakika 1:06:42.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: