Akizungumza na mwandishi wetu, baba mzazi wa mtoto huyo, Mustapha
Makombe alisema kuwa mtoto wake anateseka na ugonjwa wa kansa ya ngozi tangu akiwa na umri wa mwaka mmoja.
Makombe alisema kuwa ugonjwa huo ulianza kama
malengelenge akiwa na umri huo na wakawa wanaenda hospitali
ndogo ndogo lakini baadaye wakaamua kumpeleka hospitali ya furaa ya Muhimbili ambapo walipewa
barua yenye maelekezo kwenda hospitali ya CCBRT ambako ndiko walikogundua kuwa mtoto wake ana
kansa ya ngozi hatua ya nne.
“Baada ya kuhangaika katika hospitali
nyingi bila mafanikio, nikaamua kwenda Hospitali ya Regency (Dar) kuomba
msaada wa kwenda kutibiwa India.
“Pale waliniambia nichangie shilingi milioni moja na laki tano kwa ajili ya tiketi na viza ili mwanangu akatibiwe India, hizo hela mimi sina.
Naomba Watanzania
mnisaidie hata kwa fedha za mitandao kwa namba 0769 517765 na 0715
424697 ili niweze kumpeleka mwanangu India akatibiwe,” alisema Makombe.
0 comments:
Post a Comment