Mwili wa Erasto Msuya (kulia) baada ya kupigwa risasi. Kushoto ni gari alilokuwa anatumia.
Wanausalama wakiubeba mwili wa marehemu Msuya.
MOSHI/ARUSHA
JESHI la Polisi nchini limesema mauaji ya mfanyabiashara tajiri wa madini wa Mirerani, Erasto Msuya yalipangwa na baadhi ya wafanyabiashara wa madini ya Tanzanite kwa lengo la kulipiza kisasi.
JESHI la Polisi nchini limesema mauaji ya mfanyabiashara tajiri wa madini wa Mirerani, Erasto Msuya yalipangwa na baadhi ya wafanyabiashara wa madini ya Tanzanite kwa lengo la kulipiza kisasi.
Kauli hiyo imetolewa jana na Kamanda wa Polisi
Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz ambaye pia alimtaja mfanyabiashara
tajiri wa madini kuwa ni miongoni mwa watu waliokam
atwa hadi sasa.
atwa hadi sasa.
Mfanyabiashara huyo aliuawa kwa kupigwa risasi
nyingi kwa bunduki ya kivita aina ya Sub Machine Gun (SMG) Agosti 7
mwaka huu eneo la Mijohoroni wilayani Hai Kilimanjaro, ambapo katika
eneo la mauaji hayo lilipo hatua zipatazo 70 kutoka barabara kuu ya
Moshi-Arusha, yaliokotwa maganda 21 ya risasi za SMG lakini inaelezwa
risasi zilizompata zilikuwa ni 12.
Wakati polisi wakimshikilia mtu anayedaiwa
kuhusika na tukio hilo, watu wanaosadikiwa kuwa majambazi wamevamia
nyumbani kwa bilionea mwingine Arusha kupora kiasi kikubwa cha pesa
kabla ya kumfyatulia risasi mlinzi na kusababisha kifo chake.
Kamanda Boaz aliwataja wanaoshikiliwa kuwa ni
pamoja na mfanyabiashara Shariff Mohamed Athman (31) Mkazi wa Kimandolu
na dereva aitwaye Mussa Mango (30) Mkazi wa Shangarai Arusha.
Kwa mujibu wa Kamanda Boaz, mwingine aliyekamatwa
ni Shwaibu Jumanne Said(38) maarufu kwa jina la Mredii, Mkazi wa
Mererani Wilaya ya Simanjiro katika Mkoa wa Manyara.Kamanda Boaz
alikataa kueleza ushiriki wao akisema hilo lingeweza kuathiri uchunguzi
unaoendelea wa mauaji hayo yaliyotikisa miji ya Arusha, Mererani na
Moshi. CHANZO MWANANCHI
0 comments:
Post a Comment