BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

SAKATA LA WAZIRI WA UCHUKUZI DK HERRISON MWAKYEMBE JUU YA KUANZA KUPAMBANA KUBOMOA MTANDAO WA MADAWA YA KULEVYA APEWE ULINZI MKALI.

KAMA kuna jambo ambalo halina ubishi miongoni mwa wananchi hivi sasa ni suala la Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe kustahili kuitwa ‘Askari wa Mwavuli’ kutokana na uwajibikaji wake katika kutekeleza majukumu aliyopewa na mamlaka iliyomteua kushika wadhifa wa uwaziri.

Tumekuwa tukifuatilia kwa karibu sana utendaji wake wa kazi tangu alipoteuliwa kuwa Naibu Waziri katika Wizara ya Ujenzi baada ya Uchaguzi Mkuu uliopita hadi alipop
ewa dhima ya kuongoza Wizara ya Uchukuzi Januari 2011. 

Katika muda huo, hatukupata kutilia shaka utendaji na utekelezaji wake wa majukumu mazito aliyokabidhiwa na mkuu wa nchi, wala kuhoji dhamira na ujasiri wake katika kufikia malengo yaliyowekwa bila woga wala upendeleo.

Hata hivyo, lazima tukiri kwamba uwajibikaji na ujasiri wake katika utendaji wa kazi zake umejidhihirisha hasa baada ya kupewa fursa ya kuongoza Wizara ya Uchukuzi. 

Kusema kweli hakuna naibu waziri katika wizara yoyote ulimwenguni anayeweza kutegemewa kuonyesha makucha yake halisi ya kiutendaji, kwani kimfumo anakuwa chini ya waziri na anategemewa kutekeleza majukumu anayopewa na waziri ambaye ndiye kiongozi wake. Vinginevyo, atalalamikiwa kwa kutaka kumfunika waziri na ataibua hisia kwamba anataka kukalia kiti chake.

Tumesema yote hayo katika kujaribu kuonyesha kwa nini Waziri Mwakyembe amejipambanua zaidi kama Askari wa Mwavuli baada ya kuwa kiongozi mkuu wa Wizara ya Uchukuzi wakati hakuweza kuwa hivyo wakati alipokuwa Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi. 

Wizara ya Uchukuzi ni moja ya wizara chache nyeti hapa nchini ambazo zinashikilia uchumi wa nchi yetu na maisha ya kila siku ya wananchi. Hivi maisha pasipo vyombo vya usafiri wala miundombinu ya kuviwezesha vyombo hivyo kufanya kazi yangekuwa maisha ya namna gani?

Ni wizara nyeti kwa tafsiri yoyote ile, kwani ndiyo inayosimamia usafiri wa reli, anga, maji na barabara, pia ndiyo inayosimamia taasisi zinazoendesha bandari, viwanja vya ndege na miundombinu ya reli. 

Ndiyo maana mawaziri waliomtangulia walishindwa kuhimili vishindo, changamoto na mikikimikiki itokanayo na majaribu yatokanayo na shughuli za wizara hiyo. 

Wengi walikosa ubunifu, ujasiri na uthubutu wa kujaribu, hivyo wakaendekeza urasimu wa kusoma taarifa za mafaili katika ofisi zenye viyoyozi.

Hakuna asiyejua nini kilitokea baada ya Waziri Mwakyembe kupewa wizara hiyo. Kwanza alitangaza vita dhidi ya ufisadi, rushwa na ubadhirifu katika wizara hiyo na taasisi zote zilizo chini yake. Sote ni mashahidi wa nini kilitokea katika bandari zetu, Shirika la Ndege, Shirika la Reli, Sumatra na viwanja vya ndege.

Kama tulivyoshuhudia katika matukio mbalimbali kama wizi wa kontena na mafuta bandarini au upitishaji wa dawa za kulevya katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, ufisadi na wizi katika sehemu hizo pia umewahusisha baadhi ya watumishi katika vyombo vya ulinzi na usalama, likiwamo Jeshi la Polisi na Usalama wa Taifa.

Waziri Mwakyembe amepambana na wahalifu hao bila woga na ndiyo maana wananchi wengi wanataka apewe ulinzi wa uhakika. Kwa mfano, vita yake dhidi ya dawa za kulevya bila shaka imemtengenezea maadui wengi, tena wenye fedha. 

Tunamshauri Rais Jakaya Kikwete siyo tu ampe ushirikiano, bali pia ulinzi wa uhakika dhidi ya mafisadi, magwiji wa unga na wahalifu wengine wengi. MWANANCHI
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: