BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MABONDIA FRANCIS CHEKA NA CHIOTCHA CHIMWENE KUONDOA UBISHI PAMBANO LA MASUMBWI SUPER MIDDLE JAMHURI MOROGORO LEO.

http://t2.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcTifvjF1SsnHlxlnNpXzsAWE6zzTrT7wWnCcJsIPUGJaQzXR7Nv
FRANCIS CHEKA (SMG).https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhF0KxuSTWFooas_Qm93aOTNYjrHwmp2qCjTNwU4Tp9M7mwd5eAOiRcayWf_KUI2hA_8mByrzm02CC2CqSqEbqgn6U8eRbfvCYmOQhIsN5-5XHNZFsZ0ZuN6coaCOC-HAunLCuf0t8PAYs/s640/Chimwemwe+Malawi.JPGChiotcha Chimwemwe.

BONDIA namba moja hapa nchini, Francis ‘SMG’ Cheka amewatoa hofu mashabiki wake na kusema amejipanga kumchapa mpinzani wake, Chiotcha Chimwemwe kutoka Malawi leo hii.
Cheka aliyasema hayo jana katika mahojiano na gazeti hili mara baada ya zoezi la kupima uzito na afya kwenye ukumbi wa Hoteli ya Blue Room mjini hapa.
“Ni lazima nishinde ili kulinda heshima yangu, najua litakuwa pambano gumu lakini Chimwemwe hawezi kunipiga,” alisema Cheka.
Jioni hii Cheka na Chimwemwe wanam
aliza ubishi wa nani mkali baina yao kwenye Uwanja wa Jamhuri katika pambano la uzani wa ‘Super Middle’ raundi nane.
Katika zoezi la kupima uzito, Chimwemwe alikuwa na kilo 73, huku Cheka akiwa na kilo 75, uzito ambao Chama cha Ngumi za Kulipwa cha PST kimeeleza hauna tatizo.
Pambano la Cheka limebeba hisia za mashabiki wengi wa bondia huyo, ambapo baadhi wanaamini atashinda.
Pambano la leo litakuwa la pili kuwakutanisha Cheka na Chimwemwe, ambapo pambano la kwanza Cheka alishinda kwa pointi za majaji 2-1 mwaka jana jijini Arusha.
Kwa mujibu wa promota wa pambano hilo, Zumo Makame milango ya Uwanja wa Jamhuri itakuwa wazi kuanzia saa nane mchana.
Makame alisema bingwa wa zamani wa dunia wa WBU, Rashid Matumla atazichapa na Maneno Oswald kwenye uzani wa super middle.MWANANCHI
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: