MAHAKAMA ya Misri imeamuri dikteta Hosni Mubarak kuachiliwa huru baada
ya mahakama hiyo kusema kuwa hakupatwa na hatia katika kesi iliyokuwa
imebakia ya ubadhilifu.
Kwa mujibu wa wakili wake na duru za mahakama za
Misri, leo Jumatatu korti imeamuru Mubarak aachiliwe huru katika kesi
ambayo yeye na watoto wake wawili Alaa na Gamal walikuwa wakituhumiwa
kufanya ubadhilifu wa fedha za umma.
Taarifa hiyo inasema kwamba,
Mubarak anaweza kuachiliwa huru wiki hii, lakini watoto wake wawili
wataendelea kushikiliwa.
Huko nyuma pia iliamriwa kwamba dikteta huyo wa
Misri aachiliwe huru katika kesi nyingine mbili ambapo alishitakiwa
kuhusika katika mauaji ya waandamaji wakati wa harakati za maandamano ya
mwaka 2011 ambayo yalimuaondoa madarakani na pia kujilimbikizia mali
kinyume cha sheria.
Wamisri wengi wanaamini kuwa Mubarak aliyekuwa
kibaraka mkubwa wa Marekani na Israel wakati wa utawala wake anapaswa
kuhukumiwa kifo kutokana na kuwaua waandamanaji.CHANZO http://kiswahili.irib.ir
0 comments:
Post a Comment