Wanawake
hao vikongwe mtu na mtoto wake ni Jadi Temi (90) na mwanae Samara
Mathias (70) wakazi wa kijiji cha Ikonda wilayani Shinyanga.
Wawili
hao walishambuliwa na kuuawa juzi na watu wasiojulikana wakiwa wamekaa
nje ya nyumba yao wakiota moto na kufurahi chakula cha usiku.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Shinha Kihenya Kihenya, alisema vikongwe
walishambuliwa na mapanga sehemu mbalimbali za miili yao na kufa papo
hapo huku baadhi ya viungo vya Samara vikitupwa kwenye moto uliokuwa
jirani.
Kihenya
alisema tukio hilo lilitokea Ijumaa saa 2:00 usiku katika kijiji cha
Ikonda wilayani Shinyanga, wakati wawili hao wanaoishi peke yao wakila
chakula na kuota moto.
Kihenya
alifafanua kuwa mara baada ya kushambulia na kuua wauaji hao wakikata
kichwa cha Samara, kiganja cha mkono wa kushoto na mguu wa kulia na
kuvitupa kwenye moto uliokuwa jirani.
Alisema wauaji hawakuiba chochote na kuna wasiwasi kuwa mauaji hayo yayamefanywa kutokana na ushirikina .
0 comments:
Post a Comment