Rachel
Balama na Anneth Kagenda.
SIKU chache baada ya Katibu wa
Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini kudai jeraha alilonalo katika bega la
kulia limetokana na risasi aliyopigwa na polisi mkoani Morogoro, baadhi ya
Waislamu nchini wametoa tamko la kumtaka Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt.
Emmanuel Nchimbi, ajiuzulu mara moja.
Msimamo
huo umetolewa Dar es Salaam jana katika kongamano la Waislamu ambalo
lilifanyika katika Uwanja wa Mwembe
Yanga.Akizungumza
katika kongamano hilo ambalo lilihudhuriwa na mamia ya waum
ini wa dini
hiyo, mmoja wa viongozi wa jumuiya hiyo Shekhe Kondo Juma Bungo, alisema
Waislamu wanatoa muda kwa Dkt. Nchimbi kujiondoa katika nafasi hiyo.
Alisema,
mbali na Dkt. Nchimbi, walisema Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro,
Faustine Shilogile, anapaswa kukamatwa na kufikishwa mahakamani wakidai ndiye
mhusika mkuu wa kupanga mikakati ya kumdhuru Shekhe Ponda.
“Askari
aliyempiga risasi Shekhe Ponda na Kamanda ambaye alisimamia suala zima la uvamizi
kwa kiongozi wetu, wote wanapaswa kuwajibishwa.
tunataka
iundwe tume huru ya uchunguzi badala ya timu
iliyoundwa na polisi,” alisema.
Al i o n
g e z a k uwa , kama maazimio hayo yatapuuzwa na
wahusika
pamoja na Serikali kushindwa kuchukua hatua stahiki, itakuwa mwanzo na
mwisho wa historia ya Tanzania.
“Kitakachotokea
baada ya hapo, Serikali itaona mwanzo tu lakini haitajua mwisho
wake...Waislamu nchi nzima
watafanyamaandamano, polisi wanategemea kupandishwa vyeo au kupewa posho nyingi pale yanapotokea matatizo ya
Waislamu. “Kwa sasa hali inavyoonesha watapandishwa vyeo kwa uchungu kwani Waislamu hatutakubali,” alisema Shekhe
Bungo na kusisitiza kuwa, Shekhe Ponda ana thamani kubwa sana kwa Waislamu.
watafanyamaandamano, polisi wanategemea kupandishwa vyeo au kupewa posho nyingi pale yanapotokea matatizo ya
Waislamu. “Kwa sasa hali inavyoonesha watapandishwa vyeo kwa uchungu kwani Waislamu hatutakubali,” alisema Shekhe
Bungo na kusisitiza kuwa, Shekhe Ponda ana thamani kubwa sana kwa Waislamu.
Shekhe
Bungo alilihadharisha Jeshi la Polisi kuacha kuwatisha Waislamu na
kuongeza kuwa, Serikali isije kuwalaumu kwa kitakachotokea kama madai yao
hayatatekelezwa.
Aliwataka
Waislamu popote walipo, kutoa adhabu palevion gozi au wanachama wa Cha
maChaMapinduzi (CCM),wanapoingia misikitinina kufanya kampeni za kuomba
wachaguliwe katika uchaguzi ujao.
Tamko la
CUF
Katika
hatua nyingine,Chama cha Wananchi (CUF), kimelitaka Jeshi la Polisi
nchini,limuachie Shekhe Ponda aweze kuendelea na matibabu katika Taasisi ya
Tiba ya Mifupa (M OI)
.
Chama
hicho kimesema kitendo alichofanyiwa Shekhe Ponda cha kuondolewa MOI
wakati hali yake kiafya haijatengemaa, sichakibinadamu bali cha kinyama.
Mwenyekiti
wa chama hicho Taifa,Profesa Ibrahim Lipumba,
aliyasema
hayo Dar esS alaam jana wakati akizungumza na
waandishi
wahabari.
"Kauli
za vitisho na ubabe unaofanywa na Kamanda wa Polisi, Kanda Maalumu ya Dar
es Salaam, Kamishna Suleiman Kova, vinachochea hasira na jazba za wananchi
wengine wakiamini kuwa, jeshi hilo lina lengo la kumuua Shekhe Ponda
badala ya polisi kujenga amani, wao wanaibomoa," alisema.
Prof.
Lipumba alisema, jeshi hilo limeshindwa kufanya kazi kwa weledi ndio
sababu ya kuongezeka vitendo vya uhalifu na tuhuma nyingi kwa baadhi ya
polisi ambao wanashirikiana na wahalifu.
"Polisi
wetu wameweka pembeni kazi yao ya kupambana na uhalifu... wanapoteza
wakati mwingi na raslimali
kumshughulikia Shekhe Ponda hivyo nawaomba Watanzania wote tudai jeshi lenye weledi na linalowajibika," alisema.
kumshughulikia Shekhe Ponda hivyo nawaomba Watanzania wote tudai jeshi lenye weledi na linalowajibika," alisema.
Alisema
CUF kinaungana na Watanzania wote kulaani vikali
kitendo
alichofanyiwa Shekhe Ponda, kumfungulia mashtaka na kumuondoa MOI
alipokuwa akipatiwa matibabu bila taarifa na kumpeleka gerezani Segerea.
Aliongeza
kuwa, jeshi hilo ndio chanzo cha wananchi kuvunja
amani
ya nchi ambapo juzi mchana, alikwenda Segerea kumuona Shekhe Ponda ambapo
Mkuu wa gereza hilo alimpa ushirikiano mzuri uliofanikisha amuone na
kuzungumza naye.
" Ta
y a r i S h e k h e P o n d a amepelekewa dawa zake gerezani na amepewa huduma
za tiba zinazoweza kupatikana katika gereza hilo," alisema Prof.
Lipumba na kuongeza kuwa, taarifa alizonazo X-ray imeonesha risasi
aliyopigwa imepita karibu na mfupa ambao umepasuka.
Alisema
hali ya Shekhe Ponda inaendelea vizuri ukilinganisha
na
awali baada ya kufikishwa gerezani kwani anaweza
kutembea mwenyewe, anafahamu kamili na waliweza kutaniana na mkuu wa gereza ambaye alimhakikishia kupata huduma nzuri.
kutembea mwenyewe, anafahamu kamili na waliweza kutaniana na mkuu wa gereza ambaye alimhakikishia kupata huduma nzuri.
Prof.
Lipumba aliongeza kuwa, anazo taarifa kuwa Jeshi la Polisi mkoani Morogoro
linataka kumhoji daktari aliyemtibu Shekhe Ponda, siku alipopigwa risasi.
"Inasikitisha
kwamba polisi hawajapitia Taasisi ya Chama cha Madaktari Tanzania (MAT),
ili iombe kibali cha kufanya hivyo badala yake wanataka kumsulubu daktari
kwa kosa la kumtibu Shekhe Ponda jambo ambalo linashangaza," alisema.
Aliongeza
kuwa, CUF inataka Serikali iunde tume huru ambayo itaongozwa na Jaji ili
kuchunguza tukio la kupigwa risasi Shekhe Ponda, askari aliyempiga na waliompa
amri ya kufanya hivyo wafikishwe mahakamani na kumfutia kesi ya uchochezi.
Shekhe
Ponda alipata mkasa huu Agosti 10 mwaka huu mkoani Morogoro muda mchache baada ya kushiriki katika Kongamano la Baraza
la Eid. CHANZO http://mambomseto88.blogspot.com
0 comments:
Post a Comment