BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

SAKATA LA SHEKHE PONDA:WAISLAMU WAMTAKA DKT. EMMANUEL NCHIMBI AJIUZULU.



 
Rachel Balama na Anneth Kagenda.
SIKU chache baada ya Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini kudai jeraha alilonalo katika bega la kulia limetokana na risasi aliyopigwa na polisi mkoani Morogoro, baadhi ya Waislamu nchini wametoa tamko la kumtaka Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt. Emmanuel Nchimbi, ajiuzulu mara moja.
Msimamo huo umetolewa Dar es Salaam jana katika kongamano la Waislamu ambalo lilifanyika katika Uwanja wa Mwembe

Yanga.Akizungumza katika kongamano hilo ambalo lilihudhuriwa na mamia ya waum
ini wa dini hiyo, mmoja wa viongozi wa jumuiya hiyo Shekhe Kondo Juma Bungo, alisema Waislamu wanatoa muda kwa Dkt. Nchimbi kujiondoa katika nafasi hiyo.

Alisema, mbali na Dkt. Nchimbi, walisema Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro, Faustine Shilogile, anapaswa kukamatwa na kufikishwa mahakamani wakidai ndiye mhusika mkuu wa kupanga mikakati ya kumdhuru Shekhe Ponda.

“Askari aliyempiga risasi Shekhe Ponda na Kamanda ambaye alisimamia suala zima la uvamizi kwa kiongozi wetu, wote wanapaswa kuwajibishwa.

tunataka iundwe tume huru ya uchunguzi badala ya timu 
iliyoundwa na polisi,” alisema.
  
Al i o n g e z a k uwa , kama maazimio hayo yatapuuzwa na

wahusika pamoja na Serikali kushindwa kuchukua hatua stahiki, itakuwa mwanzo na mwisho wa historia ya Tanzania.

“Kitakachotokea baada ya hapo, Serikali itaona mwanzo tu lakini haitajua mwisho wake...Waislamu nchi nzima

watafanyamaandamano, polisi wanategemea kupandishwa vyeo au kupewa posho nyingi pale yanapotokea matatizo ya
 Waislamu. “Kwa sasa hali inavyoonesha watapandishwa vyeo kwa uchungu kwani Waislamu hatutakubali,” alisema Shekhe

 Bungo na kusisitiza kuwa, Shekhe Ponda ana thamani kubwa sana kwa Waislamu. 

Shekhe Bungo alilihadharisha Jeshi la Polisi kuacha kuwatisha Waislamu na kuongeza kuwa, Serikali isije kuwalaumu kwa kitakachotokea kama madai yao hayatatekelezwa.

Aliwataka Waislamu popote walipo, kutoa adhabu palevion gozi au wanachama wa Cha maChaMapinduzi (CCM),wanapoingia misikitinina kufanya kampeni za kuomba wachaguliwe katika uchaguzi ujao.

Tamko la CUF
Katika hatua nyingine,Chama cha Wananchi (CUF), kimelitaka Jeshi la Polisi nchini,limuachie Shekhe Ponda aweze kuendelea na matibabu katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa (M OI)
 .

Chama hicho kimesema kitendo alichofanyiwa Shekhe Ponda cha kuondolewa MOI wakati hali yake kiafya haijatengemaa, sichakibinadamu bali cha kinyama.

Mwenyekiti wa chama hicho Taifa,Profesa Ibrahim Lipumba,
aliyasema hayo Dar esS alaam jana wakati akizungumza na
waandishi wahabari.

"Kauli za vitisho na ubabe unaofanywa na Kamanda wa Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova, vinachochea hasira na jazba za wananchi wengine wakiamini kuwa, jeshi hilo lina lengo la kumuua Shekhe Ponda badala ya polisi kujenga amani, wao wanaibomoa," alisema.

Prof. Lipumba alisema, jeshi hilo limeshindwa kufanya kazi kwa weledi ndio sababu ya kuongezeka vitendo vya uhalifu na tuhuma nyingi kwa baadhi ya polisi ambao wanashirikiana na wahalifu. 

"Polisi wetu wameweka pembeni kazi yao ya kupambana na uhalifu... wanapoteza wakati mwingi na raslimali
 kumshughulikia Shekhe Ponda hivyo nawaomba Watanzania wote tudai jeshi lenye  weledi na linalowajibika,"  alisema.


Alisema CUF kinaungana na Watanzania wote kulaani vikali
kitendo alichofanyiwa Shekhe Ponda, kumfungulia mashtaka na kumuondoa MOI alipokuwa akipatiwa matibabu bila taarifa na kumpeleka gerezani Segerea.

Aliongeza kuwa, jeshi hilo ndio chanzo cha wananchi kuvunja
 amani ya nchi ambapo juzi mchana, alikwenda Segerea kumuona Shekhe Ponda ambapo Mkuu wa gereza hilo alimpa ushirikiano mzuri uliofanikisha amuone na kuzungumza naye.

" Ta y a r i S h e k h e P o n d a amepelekewa dawa zake gerezani na amepewa huduma za tiba zinazoweza kupatikana katika gereza hilo," alisema Prof. Lipumba na kuongeza kuwa, taarifa alizonazo X-ray imeonesha risasi aliyopigwa imepita karibu na mfupa ambao umepasuka. 

Alisema hali ya Shekhe Ponda inaendelea vizuri ukilinganisha
 na awali baada ya kufikishwa gerezani kwani anaweza

kutembea mwenyewe, anafahamu kamili na waliweza kutaniana na mkuu wa gereza ambaye alimhakikishia kupata huduma nzuri. 

Prof. Lipumba aliongeza kuwa, anazo taarifa kuwa Jeshi la Polisi mkoani Morogoro linataka kumhoji daktari aliyemtibu Shekhe Ponda, siku alipopigwa risasi.

"Inasikitisha kwamba polisi hawajapitia Taasisi ya Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), ili iombe kibali cha kufanya hivyo badala yake wanataka kumsulubu daktari kwa kosa la kumtibu Shekhe Ponda jambo ambalo linashangaza," alisema.

Aliongeza kuwa, CUF inataka Serikali iunde tume huru ambayo itaongozwa na Jaji ili kuchunguza tukio la kupigwa risasi Shekhe Ponda, askari aliyempiga na waliompa amri ya kufanya hivyo wafikishwe mahakamani na kumfutia kesi ya uchochezi.

Shekhe Ponda alipata mkasa huu Agosti 10 mwaka huu mkoani Morogoro muda mchache baada ya kushiriki katika Kongamano la Baraza la Eid. CHANZO http://mambomseto88.blogspot.com
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: