DAR ES SALAAM.
MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba amesema kabla ya kuundwa kwa Katiba Mpya sheria zote zinazokandamiza uhuru wa habari zitaangaliwa kwa sababu katiba ni sheria mama na sheria yoyote itakayopingana na katiba ni batili.
MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba amesema kabla ya kuundwa kwa Katiba Mpya sheria zote zinazokandamiza uhuru wa habari zitaangaliwa kwa sababu katiba ni sheria mama na sheria yoyote itakayopingana na katiba ni batili.
Kwa muda mrefu kumekuwa na malalamiko kutoka kwa
wadau wa tasnia ya habari kuhusu sheria mbalim
bali ambazo zimekuwa zikikandamiza uhuru wa habari.
bali ambazo zimekuwa zikikandamiza uhuru wa habari.
Akizungumza jana wakati wa mkutano ulioandaliwa na
Baraza la Habari Tanzania (MCT) kujadili rasimu ya Katiba Mpya, alisema
Katiba ni sheria mama hivyo sheria yoyote itakayopingana na katiba
itakuwa ni batili.
Alivitaka vyombo vya habari nchini kusikiliza
maoni ya wananchi ili kuepuka kupata katiba ya makundi kwani haitakuwa
imemaliza tatizo lililosababisha kuunda Katiba Mpya.
“Nafasi ambayo tasnia ya habari itapata kwenye
katiba itasaidia kujenga taifa kwa sababu tasnia hii ni ya pekee
inayoweza kujenga taifa endapo itatumiwa vizuri kwa kuwasilisha maoni ya
wananchi katika uundaji wa katiba na kutengeneza katiba inayokidhi haja
za wananchi na kutetea haki zao na hasa walioko vijijini,” alisema
Warioba.
Kuhusu suala la Serikali tatu Mwenyekiti huyo
alisema “Tumechambua kwa makini tukaweka Serikali tatu sasa wananchi
mtuambie ni sawa au si sawa na kama siyo sawa tufanyeje, hayo ndiyo
tunayohitaji,”.
Naye Meneja Programu MCT, Pili Mtambalike alisema
wanahabari wamepewa fursa ya kujadili na kutoa maoni yanayohusu uhuru wa
vyombo vya habari kwa kuzingatia kanuni elekezi kama uhuru wa vyombo
vya habari, na haki ya msingi ya kupokea, kuchakata na kusambaza habari,
ni mali ya umma kwa pamoja na mtu mmoja mmoja. MWANANCHI
0 comments:
Post a Comment