BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

TIMU NNE ZA LIGI KUU NA DARAJA LA KWANZA ZAJINOA NA MICHEZO YA KIRAFIKI KWA AJILI YA MSIMU WA MWAKA 2013/2014 MOROGORO.

 
MSHAMBULIAJI WA POLISI MORO SC MESHACK SELEMAN AMBAPO TIMU YAKE IPO KATIKA LIGI DARAJA LA KWANZA MSIMU WA MWAKA 2013/2014.

Na Juma Mtanda, Morogoro.
Timu nne za Morogoro zinashiriki Ligi Kuu na L ligi daraja la Kkwanza Tanzania Bbara msimu huu zipo katika maandalizi makali.
Akizungumza na gazeti hili mjini hapa, Katibu Mtendaji wa chama cha soka Mmkoa wa Morogoro (MRFA) Hamis Semka alisema timu za mkoa huo zinazosh
iriki ligi kuu na daraja la kwanza Tanzania bara zipo katika maandalizi ya mwisho.
Semka alisema kwa sasa Mmkoa wa Morogoro una jumla ya timu nne ambazo ni Mtibwa Sugar ya Manungu Turiani, inayoshiriki ligi kuu, huku Polisi Moro, Burkina Fc na Mkamba Rangers zote zipo ligi daraja la kwanza.
“Msimu wa mwaka 2012/2013 Morogoro tulikuwa na timu mbili za ligi kuu ikiwemo Mtibwa Sugar na Polisi Moro SC na katika ligi daraja kwanza nazo zilikuwa mbili za Mkamba Rangers na Burkina FC, lakini hakuna iliyofanikiwa kupanda daraja na kucheza ligi kuu zaidi ya Polisi Moro SC kushuka daraja.”
Kwa sasa ligi daraja la kwanza kwa msimu wa mwaka 2013/2014 kuna timu tatu baada ya Polisi Moro SC kuongeza idadi katika ligi hiyo kufuatia kucheza msimu mmoja tangu ipande daraja na kucheza ligi kuu huku Mtibwa Sugar ikibakiwa na pekee katika ligi kuu.
Semka alisema kuwa katika maandalizi ya mwisho kabla ya kuingia katika ligi hizo chama cha soka kimeandaa michezo ya kirafiki kwa timu zote za kujipima nguvu huku Mtibwa Sugar ikicheza mchezo wake dhidi Prinson katika uwanja wa Jamhuri Morogoro (jana) juzi katika mchezo uliomalizika kwa sare tasa ya 0-0.
“Leo (jana) timu ya Burkina FC inayoshiriki ligi daraja la kwanza ilitarajiwa kucheza na Prison, Polisi Moro SC ikijiwinda na Mbeya City ya Jijini Mbeya iliyopanda ligi kuu msimu huu katika Uwanja wa jamhuri Morogoro katika mchezo utaopigwa Agosti 13 wakati Agosti 14 Mkamba Rangers nayo itacheza na Prinson katika Uwanja wa CCM Mkamba,” alisema Semka.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: