BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

WAAMUZI CHIPUKIZI WA KITUO CHA MOROSP KUCHEZESHA LIGI DARAJA TATU NA NNE MSIMU WA MWAKA 2013/2014 NGAZI YA TFF MKOA WA MOROGORO.


Mwamuzi chipukizi Fikiri Magari (19) moja ya michezo ya waamuzi wa Morosp akiwajibika.

Na Juma Mtanda, Morogoro.
JUMLA ya waamuzi chipukizi nane wa mchezo wa soka kutoka taasisi ya kuibua na kukuza vipaji vya waamuzi Morogoro (MOROSP) wanatarajia kuanza kuchezesha michezo ya ligi daraja la tatu na nne ngazi ya TTF taifa Manispaa ya Morogoro baada ya kuony
esha uwezo mkubwa katika kuchezesha michezo mbalimbali ya soka mkoani hapa.

Akizungumza na gazeti hili mjini hapa Mkurufunzi Morosp, Marthin Saanya alisema kuwa taasisi hiyo ina waamuzi chipukizi zaidi ya 30 wa mchezo wa soka ambao baadhi ya waamuzi hao wanatarajia kuchezesha michezo ya soka ligi daraja la tatu na nne Manispaa ya Morogoro msimu wa mwaka 2013/2014.

Saanya alisema kuwa baadhi ya waamuzi hao nane wameonyesha uwezo mkubwa katika ligi ndogo ndogo zilizopata baraka na chama cha soka wilaya ya Morogoro (MRFA) ikiwemo mitihani yao ya darasani na vitendo huku wengi wao wana uwezo wa kuchezesha ligi daraja la tatu hadi nne TTF taifa ngazi ya mkoa.

Kati ya waamuzi hao ni pamoja na Raphael Ikamba (18) Juma Shabaan (18) Fikiri Magari (19) Elly Shao (23) Raphael Elisha (18) Eick Joseph (15) Shabaan Juma (21) na Feruz Ally (13).

“Taasisi hii ina wakufunzi wawili nikiwemo mimi mwenyewe na Jesse Erasmo na tumegawana kazi ya kuwafunza mimi nawafunza mambo yote ya uwanjani na mwenzangu yeye mambo ya darasani na sifa ya waamuzi hawa chipukizi wanacheza sehemu zote mwamuzi wa kati na pembeni” alisema Saanya.

Saanya alisema kuwa kwa sasa kazi kubwa iliyopo kwa waamuzi hao ni kuwapa kuchezesha michezo mbalimbali ya ligi zinazofanyika za kugombea zawadi zikiwemo jezi, mipira, fedha, na wanyama kama mbuzi na ng’ombe ili kuwapa uzoefu kabla ya kuwachuja na kuingia katika ligi zenye ushindani.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: