BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

HIZI NDIZO TABIA ZA MNYAMA MAMBA KUANZIA MFUMO WA UZAAJI WAKE NA NAMNA ANAVYOWINDA.


MAMBA ni mnyama mwenye uwezo wa kutaga mayai kati ya 50 na 70 hivyo kuwafanya kuzaliana kwa wingi na kwamba mnyama huyu ana uwezo wa kuishi hadi miaka 300 hali ambayo inasababisha kuwa na idadi kubwa ya Mamba na wakati mwingine huleta madhara makubwa kwa binadamu endapo wanavamiwa kwenye maeneo yao bila kuchukua tahadhari.





Mamba au ngwena ni spishi kubwa za reptilia za oda Crocodilia. Mamba wanaishi majini na hupatikana maeneo mengi ya kitropiki katika Africa, Asia na Australia, Amerika. Mamba hupenda kuishi katika maji baridi kama vile maziwa, mito, ardhi tepe-tepe. 



Mamba hula hasa wanyama wenye uti wa mgongo kama vile samaki, reptilian na mamalia na wakati mwingine hata wale wasio na uti wa mgongo kama vile jamii ya konokono (moluski) na kaasi kutegemeana na aina yao hasa. 


Mamba bado ni mlolongo wa viumbe wa kale na husemekana kuwa wamekadiriwa kidogo mno, tangu enzi zile za mirosana. Wanaaminika kuwa na umri zaidi ya miaka 200, huku dinosania walitoweka mnamo miaka 65 iliyopita. Mamba wamepona na kuepuka matukio mengi sana ya kutoweka.



Mamba ni miongoni mwa wanyama wenye baiolojia ya hali ya juu tofauti na muonekano wao wa kizamani. Tofauti na reptilian wengine, wao wana ubongo wa mbele; moyo wenye vyumba vinne, sehemu ya fumbatio ifanyayo kazi kama diagramu kwa msaada wa misuli inayotumiwa kuogelea mwendo wa majini mpaka kupumua. Muonekano wa nje kwa kiasi Fulani ni ishara ya maisha yao ya majini na mwindaji. 



Maumbile ya mamba yana mfanya awe mwindaji hodari. Wana umbo lililochongoka linalowawezesha kuogelea vizuri (mamba hubana miguu yao kwenye pande zao wakati wakiogelea, na huongeza mwendokasi wao kwa kupunguza ukinzani wa maji. Miguu yao mifupi, japokuwa haitumiki kupiga kasia wawepo kwenye maji, lakini huwasaidia sana katika kukata kona za haraka na miondoko ya ghafla kwenye maji au kuanzisha mwendo. 


Mamba wanatishu ngumu, ndani na mwishoni mwa kinywa chao. Tisho hiyo huzuia maji yasipite. Tundu za pua za mamba hujifunga wakati wa kuzama majini. Ndimi za mamba haziko huru, zimeshikiliwa na tishu, na matokeo yake mamba hawaweze kutoa nje ulimi wao.


Magamba ya mamba yanaaminika kuwa na matundu yenye uwezo wa kuhisi kama ule mstari wa samaki. Matundu hayo huonekana sana kwenye taya zao za juu na chini. Uwezekano mwingine ni kuwa matundu hayo ni ya kutolea taka mwili, kwa sababu hutoa kitu kama mafuta hivi ambacho hutoa/huondosha matope. 



Mamba wana kasi sana katika mwendo mfupi, majini na hata nchi kavu. Sababu mamba hula kwa kumkamata adui, hivyo wamekuwa na meno ambayo yamechongoka vizuri, na misuli yenye nguvu inayowezesha taya zake kufunga kwa nguvu na kwa muda mrefu. Taya hizi kufunga kwa nguvu kubwa na mpaka sasa ndiyo taya zenye uwezo wa kubana/kung’ata kwa nguvu kuliko mnyama yeyote yule. 


Kani/mgandamizo wa taya za mamba ni zadi ya 340atm, ukilinganisha na 270atm ya papa na 68atm ya fisi. Hata hivyo taya za midomo ya mamba hufunguliwa kwa seti ya misuli laini na dhaifu. 


Hivyo basi mamba wanaweza kutumika kwa masomo au safari kwa kufunga tu taya zao kwa hata mipira laini. Mamba pia wana uwezo mdogo wa kugeuza shingo yao upande mpaka upande.

Mamba ni washambulizi wa kushitukiza. Husubiri mawindo, samaki au wanyama wengine wanchi kavu wasogee karibu na kisha kufanya shambulizi la ghafla. 



Wakiwa wanyama wala nyama wenye damu baridi, wana metabolismu ya taratibu sana, hivyo wanaweza kuvumilia vipindi virefu vya vifaa. Licha ya kuonekana wataratibu sana mamba ndiyo wanyama wawindaji wa hatari sana kuliko wote katika maeneo yao, na baadhi ya spishi za mamba wameonekana hata wakiwashambulia papa. 


Upekee maarufu kwa mamba ni ule wa mahusiano yake na ndege aina ya kitwitwi wa Misri. Ndege huyo hounekana kuwa ana mahusiano tegemezi ya kibailojia na mamba. Kulingana na taarifa zisizoaminika, ndege hao hula wadudu wanaodhuru kinywa cha mamba, na mamba huachama mdomo wake ili kuwaacha ndege hao wasafishe mdomo wake.




Mamba wengi wakubwa humeza mawe ambayo hufanya kazi kama farumi ya kusawazisha (kubansi) maizi wake na kusaidia kwenye kusawazisha chakula, sawa na mchanga kwa ndege. CHANZO: MALIASILI ZETU.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: