BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

CHADEMA KUJADILI MASUALA MAZITO IKIWEMO MISUKOSUKO KATIKA KIKAO CHA KAMATI KUU JIJINI DAR ES SALAAM.


Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika PICHA|MAKTABA.

DAR ES SALAAM.
KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), leo inaanza kikao chake cha siku mbili ikitarajiwa kujadili masuala mazito, hasa misukosuko iliyokikumba katika siku za karibuni.


Taarifa iliyotolewa jana na Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika ilisema kikao hicho kitakachofanyika Dar es Salaam kitapokea, kujadili na kufanya uamuzi wa masuala mbalimbali ikiwamo hali ya siasa na ripoti ya fedha.

“Suala mojawapo litakuwa kujadili mihutasari ya mikutano iliyopita na yatokanayo na mikutano hiyo, taarifa ya hali ya siasa na ripoti ya fedha,” ilisema taarifa hiyo ya Mnyika, ambaye yuko ziara ya kikazi huko Uturuki.

Pia utajadili mchakato na maudhui ya mabadiliko ya katiba, taarifa ya utekelezaji wa Programu ya Chadema ni Msingi na shughuli za kanda na taarifa ya utekelezaji wa Mpango Mkakati kuhusu maboresho.

Chadema katika mawimbi makali
Miongoni mwa mambo ambayo yanatarajiwa kujadiliwa katika kikao hicho ni mustakabali wake katika kipindi hiki ambacho kinapita katika mawimbi makali kutokana na kuibuka kwa malumbano ya waziwazi baina ya viongozi wake waandamizi na pia kusimamishwa kwa baadhi ya viongozi wa mikoani.

Matukio ya karibuni yanajumuisha malumbano kati ya Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema kuhusiana na masuala ya posho, kusimamishwa kwa Mwenyekiti wa Chadema wa Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba, kuvunjwa kwa uongozi wa Mkoa wa Mara na pia kuondolewa kikaoni kwa Mbunge wa Maswa Magharibi, John Shibuda.

Wafuatiliaji wa mambo ya siasa watakuwa wanakitazama kikao hiki kama fursa ya kuweka sawa mambo ili kiendelee kutoa ushindani kwa chama tawala.

Alipoulizwa kama matukio ya hivi karibuni yatajadiliwa katika kikao hicho, Mnyika alikataa kuingia kwa undani na badala yake alisema taarifa zitatolewa baada ya kikao.

“Niko nje ya nchi, mengine utapewa majibu kesho (leo) kwa yale ambayo yatakuwepo katika taarifa zitakazowasilishwa. Yale ambayo hayatakuwepo utajulishwa pia iwapo hayatajadiliwa,” alisema Mnyika.

Zitto na Lema
Zitto na Lema waliingia katika vita ya maneno mwanzoni mwa Novemba kuhusiana na masuala ya posho ya vikao.MWANANCHI
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: