Ndugu,jamaa na marafiki wakimwombea Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya
Katiba, Dkt. Sengondo Mvungi jana katika Uwanja wa Ndege wa Mwalimu
Nyerere kabla ya kusafirishwa kwenda Afrika Kusini kwa matibabu zaidi.
Kushoto ni Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi Bw. James Mbatia. Picha na Tume ya
Katiba.
DAR ES SALAAM.
MJUMBE wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dk Sengondo Mvungi, amepelekwa Afrika Kusini kwa matibabu zaidi kutokana na kujeruhiwa na majambazi.
DAR ES SALAAM.
MJUMBE wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dk Sengondo Mvungi, amepelekwa Afrika Kusini kwa matibabu zaidi kutokana na kujeruhiwa na majambazi.
Dk Mvungi aliondoka nchini saa 6.15 mchana jana
kwa kutumia ndege maalumu ya kubebea wagonjwa aina ya Citation 560,
Medevac kuelekea jijini Johannesburg, Afrika Kusini ambako atatibiwa
katika Hospitali ya Milpark.
Ndege hiyo pia ndiyo ilitumika kuwasafirisha
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari, Dk Steven Ulimboka na Mhariri
Mtendaji wa New Habari 2006, Absalom Kibanda wakati waliposhambuliwa na
watu wasiojulikana kwa nyakati tofauti.
Akizungumza muda mfupi kwenye Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Julius Nyerere, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia
alisema kuwa imebidi wamsafirishe nje ya nchi, ili kurahisisha matibabu
yake.
“Hali yake siyo mbaya sana na anapumua mwenyewe,
lakini tumeona tumhamishie Afrika Kusini ambako kuna huduma na vifaa vya
uhakika,” alisema Mbatia na kuongeza:
“Tunawashukuru Moi (Taasisi ya mifupa ya
Muhimbili) wamejitahidi, lakini tumeona tumhamishie Hospitali ya Milpark
ili apate msaada zaidi. Watanzania waendelee tu kumwombea,” alisema.
Mbatia pia amelitaka Jeshi la Polisi kuharakisha uchunguzi wake, ili kuwabaini watu hao na sababu ya kumdhuru Dk Mvungi.
Hali kadhalika kuchunguza mazingira ya kuibiwa kwa kompyuta na simu yake.
“IGP amenihakikishia kuwa watachunguza, lakini,
tunataka polisi wa `speed up’ (waharakishe) uchunguzi wao. Tujue lengo
la watu hao kuchukua kompyuta na simu yake, maana zilikuwa na taarifa
nyingi. Tunachohitaji ni ufanisi,” alisisitiza Mbatia.
Mbatia amewashukuru Rais Jakaya Kikwete, Makamu wa
Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Seif Sharif Hamad na viongozi wa vyama vya
siasa na taasisi za kidini, kwa kumtembelea na kumjulia hali Dk Mvungi
alipokuwa hospitalini.
Katika uwanja wa ndege, alikuwepo pia Katibu wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Asaa Mohamed pamoja na ndugu wa Dk Mvungi.
Katika safari hiyo, Dk Mvungi ameambatana na daktari wake Clement Mugisha kutoka Moi. MWANANCHI
0 comments:
Post a Comment