BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MVULANA WA MIAKA 10 ASUMBULIWA NA UVIMBE SHINGONI

article-0-1952A02200000578-825 634x424 a02f5
Mvulana mdogo wa umri wa miaka (15) ana uvimbe mkubwa Shingoni unaomsababishia kushidwa kupumua vizuri lakini madaktari bingwa wanasema anaweza kutibiwa kwa kutumia Viagra.Jose Serrano wa Ciudda d Juarez, Mexico alikuwa akiona ukuaji wa uvimbe shingoni ukikuwa kila siku na kutishia maisha yake na ushauri wa madaktari unasema oparesheni ya kawaida inaweza kuleta madhara katika sehemu muhimu ya kiungo chake (shingo).

Taarifa zinasema kuwa ugonjwa huo unajulikana kama (Lymphangioma) ni uvimbe ambao dawa yake ni Viagra ambayo ni maarufu kwa kusaidia kuongeza nguvu za kiume lakini kwa upande mwingine ni dawa ya uvimbe.Jose mwenyewe anasema kuwa ana matumaini kuwa siku moja ataweza kuishi maisha ya kawaida kama vijana wengine."Kama madaktari wanaweza kunitibu mimi itakuwa ni siku ya furaha, Napenda kuwa na afya na ningependa kuwa na uwezo wa kufanya kitu chochote nikitaka," amesemaLakini wakati mwingine anapata huzuni kwa sababu yeye ni tofauti na watoto wengine. Hadi sasa hatujapata fedha ya kumtibu," amesema baba yake Jose Ramirez.
Share on Google Plus

About Anonymous

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: