BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

NAIBU KATIBU MKUU WA CCM ATOA AMWAGA MISAADA IKIWEMO KUTOA GARI LA WAGONJWA KATA YA SHELUI IRAMBA.

Mbunge wa Iramba Maghariobi akiwatuliza wananchi wasiendelee kushangilia mafanikio yake aliyokuwa akiwaeleza hususani utekekelezaji wa Ilani ya CCM.Mwigulu Nchemba ametolea ufafanuzi wa Ujenzi wa Kituo cha kisasa cha afya kata ya Shelui wakati huo huo Mbunge huyo ametoa Gari la AMBULANCE kwa ajili ya matumizi ya wananchi wa kata ya Shelui.

 
Kabla ya kutoa taarifa ya kuwapatia gari ya Ambulance kwaajili ya wagonjwa,Mbunge huyo amechangia mifuko 30 kwaajili ya ujenzi wa kituo cha afya na huku akitoa mabati zaidi ya miatano kwaajili ya ujenzi wa nyumba za Ibada na Vituo vya afya wilaya ya Iramba.
 Hii ni sehemu ya Mamia ya wananchi waliojitokeza kwenye Mkutano wa hadhara wa Mh.Mwigulu Nchemba kata ya shelui ndani ya jimbo lake la Iramba magharibi.
 Katika hatua nyingine Mbunge wa Iramba Mh.Mwigulu Nchemba amekabidhi dawati 20 kwaajili ya shule ya msingi moja wapo hapa Shelui.Kwa dawati hizi 20 Mbunge huyo atakuwa amefikisha dawati 60 ambazo wananchi waliomba kwaajili ya kutatua swala la watoto wao kukaa chini kwa kukosa Madawati.Lakini pia Mbunge huyo amepeleka madawati zaidi ya 100 kwenye shule mbalimbali ndani ya jimbo lake kulingana na mahitaji ya shule husika.
 Mtendaji wa serikali ya Mtaa wa Shelui(kushoto) wakiwaonesha Wananchi moja ya Dawati zuri na imara sana ambazo Mh.Mwigulu nchemba ametoa kwaajili ya shule ya msingi hapa Shelui.
 Kwenye Mkutano huu wa hadhara.Mh.Mwigulu nchemba alitoa fursa kwa wananchi wake kuuliza maswali mbalimbali yanayohusu mambo ya maendeeleo ndani ya kata na jimbo lake la Iramba.Huyu ni mmoja wa vijana aliyejitokeza kutoa shukrani zake kwa Mbunge wake kwanamna alivyomsaidia kutatua matatizo yake na familia yake.Kijana huyu amewaomba wanashelui kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Mbunge wao kwasababu amekuwa bega kwa bega katika kushughulikia matatizo yao.lakini pia kijana huyu alitumia muda wake kuwaelimisha wananchi wa shelui kuwa na tabia ya kuhoji matumizi ya fedha za Mfuko wa bunge na michango mbalimbali(mapato na matumizi).
 Ilikuwa ni furaha kwa Mwigulu nchemba kuzungumza na wananchi wake kuhusu maendeleo anayowafanyia,Picha hii imepigwa wakati anacheza wimbo wa kinyiramba kufurahia namna wananchi walivyojitokeza kwa wingi kumsikiliza kwenye mkutano wake,.
 Huu ni upande mwingine wa wananchi waliofika kusikiliza mkutano wa Mbunge wao Mh.mwigulu nchemba.
 Mh.Mwigulu Nchemba amewasisitizia sana wananchi wa Shelui na Iramba kushiriki kwenye kazi za maendeleo,Kuachana kabisa na kumtegemea Mbunge kufanya kila kitu.Pia amewaomba kuhakikisha wanasimamia kidete miradi mbalimbali inayoendelea kutekelezwa ndani ya wilaya yake.Pia amewaomba vijana kujitokeza kwenye chaguzi mbalimbali mwaka ujao kwenye serikali za mitaa,Ameyasema hayo kwa kuzingatia kuwa sehemu kubwa ya wananchi wa sasa ni vijana,hivyoi vijana wana fursa ya kushiriki kwenye kazi za maendeleo kwa wingi sana,na endapo watashiriki kwenye chaguzi watakuwa wamejiwekea mazingira mazuri yakuja kuwa viongozi wakubwa baadae.
Mh.Mwigulu Nchemba akiteta jambo na Mwananchi wake akieleka kwenye jukwaa kwaajili ya kuzungmza na wananchi wake wa kata ya Shelui.
 
Na Mwandishi Wetu.
Naibu katibu CCM Tanzania Bara na Mbunge wa Iramba Mgharibi Mh.Mwigulu Nchemba leo jumapili 3/11/2013 amefanya mkutano mkubwa wa hadhara hapa Iramba kata ya Shelui akizungumza na wananchi wake kuhusu shughuli mbalimbali za maendeleo na kukabidhi madawati kwaajili ya shule pamoja na kutoa taarifa ya kununua Ambulance kwaajili ya wanaShelui ya matumizi ya kubebea wagonjwa kituo cha afya cha Shelui.
 
 
Mbunge huyo ambaye kwa muda mrefu sasa ameteka media za nchi kutokana na umahili wake wa kisiasa,akiwa amembatana na Mbunge wa Tabora Mjini amezungumza mambo mengi sana na wanashelui ikiwa pamoja na kuwapa nafasi ya kuhoji na kuuliza maswali mbalimbali ya mwendeo wa siasa na utekelezaji wa Ilani ya CCM.Mwigulu Nchemba amewapongeza sana wakazi na wananchi wa Shelui kwa namna walivyoshiriki kwenye ujenzi wa kituo cha afya ambacho yeye(mwigulu) amechangia mifuko ya cement na mabati.
 
 
Pia kwa sasa amewanunulia gari la Ambulance kwaajilya wagonjwa,Gari lipo mbioni kuletwa Shelui mapema ndani ya Mwaka huu.

Katika hatua nyingine Mbunge huyo amewaomba Wanashelui kupuuzia kelele zozote za wapinzai za kuhusu yeye,amedai kuwa wapinzani(CHADEMA) wameelekeza nguvu zao kupambana na yeye kwasababu ni tishio kwao na amekuwa mstari wa mbele kufichua maovu wanayofanya na kupanga kuyafanya.
 
 
Hivyo yeye yupo imara sana na anategemea wananchi wa Shelui hawatatoa nafasi kwa watu waaina hiyo ya CHADEMA.Mwigulu amekwenda mbali zaidi kwa kusema kuwapa nafasi wapinzani nikukaribisha vurugu,uvunjifu wa Amani katika kata yao,Wapinzani ndani ya vyama vyao wanapigana ngumi mwenyekiti kwa mwneyekiti na mmeona namna walivyosababisha kifo cha kijana pale Ndago,walivyomwagia tindikali kijana(Musa Tesha)pale Igunga n.k.alisema Mwigulu.
 
 
Vijana endeleeni kujishughulisha na kazi za maendeleo,endeleeni kujikusanya kwaajili ya kutoa misaada ya bodaboda na mikopo kama nilivyofanya kwenye kata zingine,Naomba mshiriki kwenye michezo hasa hii michuano yangu niliyoanzisha.Kukaa bila kazi ni hatari sana kwa kijana ndio maana mnakuja kujiingiza kwenye vyama visivyo na mwelekeo wowote hapa nchini"Mwigulu.
 
 
Jambo kubwa la kufurahisha katika Mkutano huu Mh.Mwigulu Nchemba alitoa nafasi kwa wananchi kutoa dukuduku zao,mawazo na maswali ya mambo mbalimbali yanayowakabili.Maswali yote yalijibiwa na mengine kujibiwa na watendaji moja kwa moja,Hatua hii imetoa fursa kwa wananchi kujua mambo mengi hasa matumizi ya mfuko wa jimbo ambapo wengi wao walikuwa hawajui kuwa Mbunge hakutani na fedha ya Mfuko wa jimbo zaidi ya Ofisi ya waziri mkuu na mkurugenzi wa wilaya na kisha kwenda kwa mfumo wa cheki kwenye serikali za vijiji.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: