BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

HII NDIYO AJALI YA LORI ILIYOTOKEA KIMARA JIJINI DAR ES SALAAM NA VIBAKA KUTAKA KUIBA MAFUTA


Displaying IMG-20140115-WA0000.jpg

Displaying IMG-20140115-WA0001.jpg
Mkuu wa Kituo cha Polisi Kimara (Mwenye shati la blue akijaribu kuzuia vijana waliokuwa wanaiba Diesel kwenye gari iliyopata ajali

Displaying IMG-20140115-WA0002.jpg

Displaying IMG-20140115-WA0003.jpg
Kufa kufaana? Vijana waliingia kazini na kuanza kuchota mafuta baada ya kuokoa majeruhi..

Ajali mbaya ya gari aina ya Lori  imetokea leo  mchana majira ya saa 7  maeneo ya Kimara. Chanzo cha habari toka eneo la tukio kimesema  ajali hii imetokea baada ya Dereva wa Lori kuwa kwenye mwendo kasi na kushindwa kuhimili breki za gari yake baada ya kukutana na kona ya gafla katika  ya vizuizi vya magari yaendayo kasi katika barabara hiyo inayoendelea na ujenzi.

ChingaOne blog ilifanya mahojiano na baadhi ya watu katika eneo la tukio na kugundua kuwa wananchi wengi wamechoshwa na ujenzi wa  bararaba hiyo iliyochukua muda mrefu ambayo kwa sasa imekuwa  kero kwa watuaji na mara nyingi baadhi ya sehemu hufungwa na kufungulia bila taarifa kiasi cha kuleta foleni na kusababisha ajali .

Baadhi ya Wananchi wa Kimara wamesema kuna haja ya Serikali kuangalia muda wa Ujenzi wa barabara hiyo inayotumika na wengi ikiwemo magari yanayofanya safari ndani na nje ya nchi, Wameomba kuhamishiwa muda wa usiku ambapo barabara inakuwa kimya na haitumiki na watu wengi ukilinganisha na muda wa mchana.

Hadi naandika habari hii kuna watu wawili wameng'ang'ania chini ya gari na bado hayajatolewa hadi sasa ila cha ajabu kundi la Vijana limevamia eneo hilo na kuanza kuiba mafuta yaliyokuwa kwenye gari lililopata ajali.http://www.chingaone.com

Endelea kuungana nasi kwa habari zaidi......
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: