BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

KOCHA MPYA WA KLABU YA YANGA AINGIA NA MIKWARA, AJIGAMBA KUMNYAMALISHA LOGARUSIC WA SIMBA SC.

Kocha mpya wa Yanga, Hans Van Der Pluijm. 


YANGA imemsainisha mkataba wa miezi sita, Mholanzi Hans Van Der Pluijm na haraka haraka kocha huyo akawaambia viongozi wa timu hiyo akisema: “Mimi ndiye kiboko ya Logarusic (kocha wa Simba), niachieni kazi mtaona nitakachofanya.”

Van Der Pluijm alisaini mkataba huo mbele ya viongozi wa Yanga jana Jumatatu saa nane mchana katika ofisi za Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji zilizopo jengo la Quality Plaza, jijini Dar es Salaam.
Kocha huyo aliwaambia viongozi wa klabu hiyo kuwa anamfahamu vizuri kocha wa Simba, Zdravko Logarusic, kuanzia falsafa yake na mbinu zake anazotumia uwanjani, hivyo ana uwezo mkubwa wa kumshinda uwanjani.
Mdachi huyo aliwataka viongozi wa Yanga kutokuwa na hofu yoyote juu yake na kuanzia sasa wanaweza kutembea kifua mbele kwa kuwa hawatakuwa na hofu ya matokeo katika mechi zinazokuja mbele yao.
Akizungumza na Mwanaspoti katika mahojiano maalumu, Van Der Pluijm, alisema rekodi yake nzuri ni ile aliyomfunga Logarusic mabao 4-1 wakiwa nchini Ghana wakati akiifundisha Berekum Chelsea na mwenzake alikuwa akiinoa Ashanti Gold.
“Namfahamu vizuri kocha (Logarusic), ni kweli nilimfunga mara ya mwisho tulipokutana, lakini sitaki kutumia matokeo hayo na kuyaleta Yanga, mpira unabadilika lakini kwa kuwa namjua mbinu zake, hawezi kunisumbua. Yanga wasiwe na wasiwasi ngoja nikatengeneze timu,” Van Der Pluijm.
Akubali majukumu
Van Der Pluijm alikiri kupewa mikakati na uongozi namna ya kuiweka Yanga katika ramani ya soka Afrika ikiwamo kuifikisha katika hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, hivyo atatumia uzoefu wake ili kuhakikisha anafanikiwa.
“Nitatumia uzoefu wangu katika soka la Afrika kutimiza matakwa ya Yanga, haya ni makubaliano yangu na uongozi. Nimeshaanza kazi rasmi ndiyo maana nakueleza hata wewe mambo haya, nimekuwa kwa muda mrefu katika kazi hii hapa Afrika. Nataka kutumia uzoefu wangu kuipa mafanikio Yanga,” alisema Van Der Pluijm.
Aweka masharti
Akizungumzia aina ya soka analotaka Yanga, Van Der Pluijm alisema anataka kuona kikosi chake kinacheza soka lenye asili ya nchi tatu zikiwemo Brazil, Uholanzi na England. MWANASPOT
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: