BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

BAADA YA MSANII CHRIS BROWN KUTUMIKIA KIFUNGO, YAELEZWA AMEKUWA AKIKATAA CHAKULA NA KUKOSA USINGIZI GEREZANI.

Chris BrownChris Brown baada ya kuvunja sheria za rehab alifukuzwa na baadae kukamatwa, hivi sasa amewekwa jela kwa muda wa mwezi mmoja.



Mtandao mmoja wa huko Marekani umeripoti kwamba Chris Brown yupo kwenye hali mbaya ndani ya gereza hilo kiasi kwamba hali chakula, usiku halali, anaongea peke yake na maisha ya humo ndani ni magumu kwake.

Wanaendelea kuripoti kwamba Chris anakunywa maji tu na wakati mwingine anapewa juisi ya machungwa. Huwa anapewa sandwich kwenye chombo kibovu na Chris Brown huwa anakataa hiyo sandwich.

Chris bado anakabiliwa na mashtaka mengine ambayo ni kumpiga kijana mmoja na kama kesi hiyo ikimuendea vibaya anaweza kwenda jela miaka 4.

Taarifa zinazotoka hivi sasa ni kwamba mwanasheria wa Chris Brown anafanya juhudi zote za kumlipa kijana huyo ili mteja wake akimaliza mwezi mmoja wa jela asiwe na kesi yoyote.

Mwezi huu mmoja anaotumikia Chris ni kutokana na jaji kumtaka akae rehab baada ya kuvunja sheria alizowekewa baada ya kesi ya Rihanna. 

Lakini pia akavunja sheria za Rehab na kujikuta anafungwa kwa mwezi mmoja.

Chris Brown - Don't Judge Me.

 

Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: