BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

TASWIRA YA MATUKIO YA PICHA ZA WAJUMBE WA BUNGE MAALUM LA KATIBA MJINI DODOMA LEO.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta na wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Bungeni mjini Dodoma Machi 3,2014. Kushoto ni Kingunge Ngombale-Mwiru, Kulia ni Freeman Mbowe na Wapili kulia ni James Mbatia. (Picha na Ofisi yaWaziri Mkuuy)
 
Waziri Mkuu,Mizengo Pinda na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, wakitoka kwenye ukumbi wa Bunge mjini Dodoma Machi 3, 2014 baada ya kusitishwa shughuli za Bunge Maalum la Katiba. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

HII TASWIRA NYINGINE YA MATUKIO MBALIMBALI KATIKA PICHA BUNGE LA KATIBA MJINI DODOMA 

Mwenyekiti wa Muda wa Bunge Maalum la Katiba Mh. Pandu Ameir Kificho akisalimiana na baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba alipowasili katika ukumbi wa Bunge leo Mjini Dodoma kushoto kwake ni Bw. Mohamed Mbwana, katikati ni Rufai said Rufai na Kulia kwa Mwenyekiti ni Bw. Heri Khatibu.

Mjumbe wa Bunge la Katiba na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Hawa Ghasia na Naibu Waziri Wizara ya Uchukuzi Charles Tizeba wakiwasili katika ukumbi wa Bunge leo Mjini Dodoma.
Mjumbe wa Bunge la Katiba na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Hawa Ghasia akitoa mapendekezo juu ya taratibu za kupiga kura katika kufanya marekesho ya kanuni zitakazotumika katika Bunge Maalum la Katiba, wakati wa Semina ya Kujadili kanuni zaitakazoongoza Bunge Maalum la Katiba leo Mjini Dodoma.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda akiwaeleza jambo Waziri wa Fedha Saada Salum Mkuya (katikati) na Makamu wa Pili wa Rais, Zanzibar Balozi Seif Ally Iddi(Kushoto). Wakati wa Semina ya Kujadili kanuni zaitakazoongoza Bunge Maalum la Katiba leo Mjini Dodoma.

Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba ambaye ni Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahim Lipumba akitoa mapendekezo yake kuhusu taratibu za upigaji kura unaoangalia maridhiano ya misingi ya kidemokrasia .Kulia ni Waziri Nchi, Ofisi ya Rais, Kazi Maalum Prof. Mark Mwandosya na mbele ni Mbunge wa Jimbo la Monduli, Edward Lowassa.wakati wa Semina ya Kujadili kanuni zaitakazoongoza Bunge Maalum la Katiba leo Mjini Dodoma.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: