UMBUMBUMBU wa wajumbe wengi wa Bunge Maalumu la Katiba kutoisoma na
kuielewa vizuri Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2013,
umesababisha kwa asilimia kubwa Bunge hilo kushindwa kuanza vikao vyake
rasmi, Tanzania Daima Jumatano limebaini.
Bunge hilo ambalo lilianza kukutana tangu Februari 18, mwaka huu,
hadi sasa limeshindwa kumchagua mwenyekiti wake wa kudumu kutokana na
kutokamilika kwa baadhi ya taratibu za awali za uendeshwaji wa uchaguzi
na vikao.
Ni siku 12 za kazi zimepita tangu wajumbe hao waanze kukutana mjini
Dodoma lakini kwa kipindi chote hicho, wameshindwa kukamilisha taratibu
za awali kutokana na kutumia muda mwingi kuzomeana, kushangilia,
kukashifiana na kuoneshana ubabe katika kufikia uamuzi na masuala
kadhaa.TANZANIA DAIMA
MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO
- Blogger Comment
- Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment