BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

CHADEMA YAJIGAMBA KAMPENI YA ZA UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE JIMBO LA KALENGA IRINGA.

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeweza kujipenyeza katika kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge wa Kalenga, kikiwa kimefanya mikutano 157 katika kata 13 ndani ya siku 10 tangu kuanza kumnadi mgombea wake, Grace Tendega. Tathmini hiyo ilitolewa jana kwa waandishi wa habari mjini hapa na Mkurugenzi wa Operesheni na Uchaguzi wa CHADEMA, Benson Kigaila, akisema idadi hiyo imefikiwa baada ya mgombea wao kufanya mikutano miwili hadi mitatu kila siku.

Kigaila alisema katika mpango kazi wao, walilenga kuzifikia kata zote 13, kazi ambayo wameifanya na kwamba sasa wameshaanza kuingia vijijini ili waweze kuvifikia vyote 71.TANZANIA DAIMA.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: