BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

HAYA NDIYO MAAJABU 12 YA SAMAKI AINA YA NYANGUMI BAHARINI.


Nyangumi ni mamalia wa bahari, au pengine wa maji matamu, katika oda Cetacea wanaofanana na samaki. Kwa hivyo hawatagi mayai kama samaki lakini huzaa watoto kama mamalia wote na huwanyonyesha.
Pamoja na nguva wanyama hawa ni mamalia wa pekee wanaoishi kwenye maji tu. Oda yao ina mnamo spishi 80. Spishi ndogo huitwa pomboo kwa kawaida na spishi kadhaa za pomboo huishi kwenye maji matamu ya mito mikubwa kama Ganges au Amazonas.

1. Moyo wa nyangumi una kilo 600, ukubwa wake ni sawa sawa na ukubwa wa gari ndogo
2.Mtoto wa nyangumi hunywa lita 400 kila siku akiwa na umri wa miezi 7 tu? 


3. Mtoto wa nyangumi ana uzito wa kilo 2700 ambayo ni sawa sawa na kifaru mkubwa size ya mwisho?

4. Uzito wa nyangumi mkubwa unakadiriwa kuwa wa tani 200 hadi 300? Mmoja JIKE alikamatwa na kupimwa alikuwa na kilo 171000kg
5. Ulimi wa nyangumi una uzito wa tani 3 ambao ni uzito zaidi ya Tembo mkubwa?
6.Mdomo wa nyangumi unaweza kuhifazi tani 90 za chakula na maji akiufumbua mpaka mwisho?

7. Chakula kikuu cha nyangumi ni dagaa kamba, ambapo nyangumi mkubwa hula dagaa kamba zaidi ya 4000000 kwa siku, ili nyangumi ashibe vizuri anakula kilo 3600kg?
8. Nyangumi anaweza kuishi mpaka kufikia miaka 80?
9.Baadhi ya mishipa ya nyangumi ni mikubwa kiasi kwamba Binadamu anaweza kuogelea ndani ya mishipa hiyo bila kugusa pembeni

10. Ukubwa wa nyangumi unaweza kulinganishwa na ndege aina ya Boeing 737
11. Urefu wa nyangumi unakadiriwa kuwa wa mita30 mpaka 50, ukimuweka ardhini urefu wake ni sawa sawa na urefu utakaojitokeza baada ya kuyapanga magari 9 ya size ya familia, Aliyekamatwa mara ya mwisho alikuwa na urefu wa mita33.
12. Nyangumi ndio mnyama mwenye sauti kubwa kuliko kitu chochote duniani. Hutoa sauti kali sana ya kipimo cha decibles188 ambayo inaweza kusikika mpaka umbali wa kilomita 848.
Ni sauti kubwa na kali kuliko sauti itoayo ndege kubwa aina ya jet inapopaa ambayo kipimo cha sauti ya jet ni decibles 120 Na King Octavian kutoka Jamii Forums.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: