BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

CHAMA CHA MAKOCHA MORO CHAFUNGA MAFUNZO YA KOZI YA AWALI MPIRA WA MIGUU KWA MWAKA 2014.

KOCHA aliyeipandisha klabu ya Mtibwa Sugar wakati huo kutoka daraja la pili hadi ligi daraja la kwanza wakati huo sasa ligi kuu Ahmed Mwarabu Mumba kushoto na Kocha aliyeipatia ubingwa wa bara mara mbili mfulululizo timu ya Mtibwa sugar, John Simkoko mwenye jezi ya bluu wakifuatilia mpambano huo nje ya. Simkoko sasa hivi ni Mwenyekiti wa Tafca na Mumba ni Katiabu.

Na Mtanda Blog, Morogoro.
Chama cha waamuzi mkoa wa Morogoro (Tafca) kimetangaza kutoa mafunzo ya mwisho ya kozi ya awali ya mpira wa miguu na kuwa kozi hiyo imeanza septemba 3 hadi 13 mwaka huu mkoani hapa.


Akizungumza na gazeti hili Katibu Mkuu wa chama cha makocha mkoa wa Morogoro, Ahmed Mumba alisema kuwa mafunzo tayari yameanza septemba 3 na yatamalizika septemba 13 mwka huu.

Kozi hiyo ni kozi ya awali ya mpira wa miguu na ndiyo itakuwa ya mwisho kwa mwaka 2014.

Mumba alisema kuwa mpaka sasa tayari chama cha makocha kimetoa mafunzo ya ngazi ya awali na kati kwa kufundisha makocha 97 katika wilaya za Ulanga, Kilombe na Manispaa ya Morogoro.

“Kozi hii itakuwa kozi ya mwisho kwa mwaka huu 2014 kwani mpaka sasa tayari tumefundisha jumla ya walimu wa soka 97 kwa ngazi ya awali 81 na ngazi ya kati 16 hili linatufanya chama kufanya kazi zaidi mwaka 2015 kuhakikisha kunakuwa na walimu wengi wa soka.”alisema Mumba.

Mumba alisema kuwa mwakani chama hicho kitahakikisha kila wilaya inakuwa na walimu wengi waliopta mafunzo ya kozi ya awali ya mpira wa miguu na kati itasaidia vijana wetu wanaelewa mbinu za soka mapema ili baadaye kusaidia taifa sambamba na kujipatia kipato kupitia mpira.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: