BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

CHANZO CHA AJALI YA MBUNGE WA MBEYA MJINI JOSEPH MBILINYI NA KUNUSURIKA KIFO CHAWEKWA BAYANA.


Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi 'Sugu' amenusu kifo baada ya gari aliyokuwa akisafiria kupata ajali katika eneo la mlima Kitonga mkoani Iringa.

Taarifa za awali kutoka kwa katibu wake, Kwame Anangisye zimeeleza kuwa Mbunge huyo akiwa na watu wanne kwenye gari yake alipata ajali hiyo mwanzoni mwa mlima Kitonga akitokea Mbeya kuelekea jijini Dar es Salaam.
 
Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi akielekeza namna ajali ilivyotokea.

“Tulipoanza kushuka kwenye mlima Kitonga gari ya Mbunge ilifeli breki na kisha kupinduka mara moja na kugeukia ilikotokea, ilikuwa ajali mbaya lakini tunashukuru Mungu tumepona.


Amesema pamoja na ajali hiyo kuonekana mbaya kwao, wanamshukuru Mungu kwani waliweza kutoka wakiwa salama na hakuna hata mmoja aliyepata maumivu makali.MWANANCHI
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: