BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MKUU WA KITUO CHA POLISI MORO ATUMIA MASAA MAWILI KUTOA USHAHIDI KESI YA SHEIKHE PONDA ISSA PONDA MAHAKAMANI.

Wafuasi wa Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikhe Ponda Issa Ponda (waliokaa chini) wakiwa chini ya ulinzi mkali wa askari polisi wakati kesi ya katibu huyo ikisikiliza kwa mara ya kwanza katika mahakama ya hakimu mkazi Morogoro jana.

Na Hamida Sharrif, Morogoro.
Kesi inayomkabili Kiongozi wa Jumuiya na Taasisi ya Kiislamu, Sheikh Ponda Issa Ponda, imeanza kusikilizwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro na shahidi wa kwanza katika kesi hiyo ni aliyekuwa Mkuu wa Polisi Wilaya ya Morogoro, Sadick Tindwa, ambaye kwa sasa amehamishiwa Wilaya ya Handeni mkoani Tanga kutoa ushahidi wake kwa zaidi ya saa mbili.


Tindwa alitoa ushahidi mbele ya ulinzi mkali nje viwanja vya mahakama hiyo iliyojaa watu wanaodaiwa kuwa wafuasi wa kiongozi huyo.


Akitoa ushahidi wake mahakamani hapo na kuongozwa na Wakili wa Serikali, Benard Kongola, Tindwa alidai kuwa Julai 31, mwaka 2013, akiwa mkuu wa polisi Wilaya ya Morogoro, alipokea barua kutoka kwa Umoja wa Wahadhiri wa Dini ya Kiislamu wakiomba kufanya Kongamano la Sikukuu ya Eid Pili kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege, Manispaa ya Morogoro, Agosti 9 mwaka 2013.


Shahidi huyo alieleza mahakamani hapo kuwa, kwa mamlaka aliyokuwa nayo alitoa kibali cha kuruhusu kongamano kwa sharti la kutotoa maneno ya kashfa dhidi ya dini nyingine na viongozi wa Serikali au maneno ya uchochezi.


Tindwa alidai kumsisitizia mwenyekiti wa kongamano hilo, Iddi Musa kufuata masharti.


Alieleza kuwa, siku ya kongamano yeye kama mkuu wa polisi wilaya na maofisa wengine, walikwenda kwenye kongamano hilo kwa lengo la kuimarisha ulinzi.


Alidai baadhi ya wahadhiri walifuata masharti waliyopewa, lakini msemaji wa mwisho, mshtakiwa Ponda Issa Ponda alitoa maneno yenye mtazamo wa uchochezi, kashfa na kuumiza imani za dini nyingine, jambo ambalo ni kinyume na kibali kilichotolewa, pia ni kosa kisheria.


Tindwa alinukuu maneno ya Ponda: “Waislamu wenzangu, tuiangalie Serikali yetu, wananchi wa Mtwara walikuwa wanadai haki yao ya gesi, lakini wamepata matatizo makubwa ya kupelekewa jeshi kwa sababu tu asilimia kubwa ya wananchi wa Mtwara ni Waislamu.


“Angalieni wananchi wa Loliondo, walikuwa wanadai haki yao ya ardhi, lakini hawakupelekewa majeshi kwa sababu asilimia kubwa ya wananchi wa Loliondo ni Wakristo.


“Pia kamati za ulinzi na usalama za dini zimeundwa na Bakwata pamoja na Serikali kwa manufaa yao binafsi, hivyo kamati hizo zikija katika misikiti yenu kujitambulisha wafungieni milango kisha wapigeni.” Kutokana na maneno hayo, alitoa taarifa kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro wakati huo, Faustine Shilogile aliyeamuru Ponda kukamatwa, lakini ilishindikana.


Upande wa utetezi ulimuuliza maswali shahidi huyo kuhusu nafasi ya Ponda katika kongamano hilo na uhusiano uliokuwapo kati ya mashtaka aliyofunguliwa na maneno aliyotoa.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: