BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

HABARI MPYA !!! VURUGU MJI MDOGO WA ILULA: MWANANCHI AFARIKI DUNIA HUKU KITUO CHA POLISI KIKICHOMWA MOTO IRINGA.

Inasemekana polisi walivamia eneo la kilabuni na kuanza kupiga kila raia na kusababisa kifo cha mama muuza Pombe za kienyeji na kufariki dunia baada ya vurugu kuzuka katika mji mdogo wa Ilalu mkoani Iringa mapema leo.


Chanzo cha vurugu hizo kinaeleza kuwa kosa lilikuwa kufungua kilabu cha Pombe kabla ya muda ulioruhusiwa kisheria.

Wananchi wamechoma magurudumu barabara Kuu ya Morogoro-Iringa na kusababisha magari kushindwa kutumia barabara hiyo huku Polisi wakilazimika kukimbia baada ya kuzidiwa nguvu na wananchi.

Baada ya tafrani hizi wananchi waliandamana na kwenda kuchoma moto kituo cha polisi.

Updated....
Baadaye gari tatu kutoka Iringa mjini zilizosheheni askari wa kutuliza ghasia (FFU) ziliwasili eneo hilo na kufyatua mabomu mfululizo kwa lengi la kutawanya wananchi na kuanza kuondoa uchafu uliokuwa umerundikwa barabarani kwa kusafisha na kuzima moto sanjari kutoa magurudumu barabarani.

Wananchi hao wamefanya uhalibifu kwa kuchoma moto magari mabovu yaliyoegeshwa katika kituo hicho.Chanzo http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/809267-vurugu-ilula-mwananchi-afariki-kituo-cha-polisi-chachomwa-moto.html
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: