BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

BASI LA LUWINZO LAPATA AJALI KWA KUGONGANA NA BASI NDOGO LA MSANGA LINE EXPRESS HIFADHI YA MIKUMI, WATU SABA WAFARIKI DUNIA PAPO HAPO, 17 WAJERUHIWA MOROGORO.

Basi la Luwinzo na basi ndogo la Masanga Line Express zimepata ajali kwa kugonga katika hifadhi ya Mikumi barabara kuu ya Iringa-Morogoro na kusababisha watu saba kupoteza maisha papo hapo huku wengine 17 wakijeruhiwa katika tukio lililotokea leo majira ya saa 6 mchana mkoani Morogoro.


Ajali hiyo ni ya pili ndani ya siku mbili baada ya ajali nyingine katika hifadhi hiyo ikihusisha basi la FM Safari na Fuso kutokea marchi 17 majira ya saa 5:30 asubuhi na kusababisha watu wawili kufariki dunia na wengine nane kujeruhiwa.


Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Morogoro Leonard Paulo alisema kuwa chanzo cha ajali hiyo kimetokana na utelezi ukichangiwa na mwendo kasi hali iliyomfanya dereva wa basi ndogo la Msanga Line Express kushindwa kulimudu vyema gari na kwenda kuligonga basi la Luwinzo lililokuwa likitokea Njombe kuelekea Dar es Salaam.

Kwa matukio ya picha za ajali hizo endelea kuungana nasi ili kuweza kuona matukio yote mawili ambayo yameghalimu maisha ya watu tisa na majeruhi 25.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: